Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 17 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 143 2022-05-06

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: -

Je, Bodi za Parole za Mkoa na Kitaifa zinakaa vikao vingapi kwa mwaka na wafungwa wangapi wamepata msamaha kwa mwaka 2020/2021?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Bodi ya Parole ya Taifa na Mikoa iliundwa kwa Sheria Na. 25 ya mwaka 1994 na ikafanyiwa marekebisho na Sheria Na. 5 ya nwaka 2002 kwa lengo la kutaka wafungwa wengi wanufaike na mpango huu. Bodi za Mikoa na Taifa kisheria zinatakiwa kufanya vikao vyake angalau mara nne kwa mwaka.

Aidha, katika kipindi cha mwaka 2020/2021 idadi ya wafungwa waliopata msamaha kupitia Bodi ya Parole nchini ni 70. Nashukuru.