Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza wataalam wa saikolojia kwenye jamii ili kutoa huduma za ushauri wa afya ya akili na namna ya kuondokana na msongo?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, ashante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa Serikali kupitia vyuo vikuu hapa nchini inatoa mafunzo ya saikolojia. Kwa nini basi isiajiri wataalamu wa saikolojia ili kupunguza tatizo hili kwa sababu kumekuwa kukiongezeka kesi za mauaji na ukatili kila kukicha?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa nini Serikali isiwe na mpango wa kusajili chama cha wataalamu wa saikolojia kama ilivyo kwa taaluma nyingine nchini kama udaktari? Ahsante.

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la kwanza ni ajira; Serikali inaendelea kushirikiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili kupata kibali kwa kuajiri wataalamu hao kadri bajeti inavyoruhusu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili kuunda bodi ya wataalamu; Serikali ipo kwenye mchakato wa kukamilisha utungaji wa Sheria ya Wataalamu wa Ustawi wa Jamii ili kuona kwamba itakapomalizika basi bodi hiyo itaundwa ili kusajili wataalamu hao wa ustawi wa jamii ikiwemo wanasaikolojia. (Makofi)

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza wataalam wa saikolojia kwenye jamii ili kutoa huduma za ushauri wa afya ya akili na namna ya kuondokana na msongo?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuwa sera ya Wizara ya Elimu inatambua umuhimu wa kuwa na walimu wanaotoa ushauri wa nasaha kwenye shule zetu.

Je, Wizara hii ya Maendeleo ya Jamii ina mpango gani wa kuhakikisha ya kwamba jambo hili linatekelezeka na kwenye shule zetu kunakuwa na walimu wanaotoa ushauri nasaha kwa watoto wetu hususan ukizingatia kwamba kuna wanafunzi wengi wanaohitimu masomo ya saikolojia na kwa kuanzia wanaweza kuanza kwa njia ya kujitolea? Ahsante.

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa wanasaikolojia hao. Kwa hiyo Serikali ipo katika kujipanga na kuhakikisha kwamba pale tunapopata nafasi za ajira basi wataalamu hao tutawaajiri na kushirikiana na Afisa wa Maendeleo ya Jamii kuwapa elimu wananchi wetu. Ahsante. (Makofi)

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza wataalam wa saikolojia kwenye jamii ili kutoa huduma za ushauri wa afya ya akili na namna ya kuondokana na msongo?

Supplementary Question 3

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa wataalamu wa saikolojia na unasihi bado ni tatizo; je, Serikali haioni imefikia wakati wakaanza kliniki tembezi ili kuweza kutembea katika maeneo mbalimbali na kutoa huduma hiyo? Ahsante.

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Toufiq kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum wapo wataalamu hao katika kila mikoa na wanafanya kazi katika Halmashauri hadi vijijini. Pale wananchi ambapo wanapata tatizo katika vijiji vyao basi wamfuate mkuu wa Kijiji. Mkuu wa Kijiji atatoa taarifa katika Halmashauri kuhakikisha wataalamu wale wanakuja kuwapa elimu ya saikolojia watoto hao. (Makofi)

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza wataalam wa saikolojia kwenye jamii ili kutoa huduma za ushauri wa afya ya akili na namna ya kuondokana na msongo?

Supplementary Question 4

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, tatizo hili ni kubwa kiasi ambacho sasa hivi watu wanaishia Mirembe badala ya kutibiwa wakiwemo wanaume wanaopigwa na wake zao, wakiwepo watoto wa shule ambao wanajeruhiwa na wenzao au na walimu.

Je, ni lini hasa Serikali itaona ni wakati muafaka wa kutoa hata mafunzo hadharani wakati wanaposhughulikia hizo ajira?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu elimu kama nilivyoeleza Wizara imejipanga kuhakikisha tunatoa elimu kwa wananchi wote hasa wale ambao wanakuja katika sehemu zetu husika wana matatizo ya saikolojia basi tunawapa elimu na tumejipanga kwamba tutakapopa wafanyakazi wengi basi elimu hiyo tutaitoa kwa kila mikoa na kuhakikisha kwamba wananchi wetu wanapata elimu hii ili kuondokana na matatizo ya saikolojia na kuondokana na msongo wa mawazo. (Makofi)