Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. BAHATI K. NDINGO K.n.y. MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha Bima za Afya za Wazee ili ziweze kutumika wakiwa nje ya Mikoa ambayo wamepewa Bima hizo.

Supplementary Question 1

MHE. BAHATI K. NDINGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza, pamoja na kwamba huduma hizi za Wazee za kutibiwa bure zinatolewa kwenye hospitali zetu, lakini tunaona wazee wetu wanapofika kwenye hivi vituo wanakosa dawa za muhimu wakati mwingine wanapata usumbufu mkubwa kulingana na umri wao. Sasa Serikali inayo mkakati gani kuhakikisha kwamba endapo dawa zinakosekana wazee hawa wanafanyiwa utaratibu maalum wa kutafutiwa dawa hizo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lingine ni kwamba tunao utaratibu ambao umekuwa ukisemwa na Serikali wa Bima ya Afya kwa wote. Je, ni lini sasa Serikali inaenda kukamilisha utaratibu huu ili wananchi wote, wazee na wengine waweze kupata huduma hii muhimu kwenye hospitali zao? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge. Moja ni kama wazee wakifika mahali, dawa haiko hospitalini ni utaratibu gani umewekwa kuhakikisha kwamba wanapata dawa bila kusumbuliwa.

Mheshimiwa Spika, kikubwa ni kwamba kuhakikisha hakuna dawa inayokosekana kwenye hospitali zetu hicho ndiyo cha kwanza. Lakini sasa hivi tunaelekeza maduka ya Bima ya Afya ambayo yako kwenye maeneo yetu ya hospitali ambayo yanaendeshwa kama private yaweze vilevile kutoa huduma hiyo kwa wazee bila kuwa-charge wakati mchakato wa bima ya afya unakuja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia suala la Bima ya Afya kwa watu wote kama alivyoelezea Waziri wa Afya hapa hivi karibuni kwamba tayari limeshafika kwenye Baraza la Mawaziri na michakato mingine ya Serikali.

Sasa Serikali imeshauri lirudi Bungeni lakini lirudi vilevile kwenye chama, kwa maana linatakiwa lije kwetu sisi Wabunge, likija kwetu Wabunge tuliangalie kwa makini yake kwa sababu kupitisha ni jambo moja, lakini je litakuwa na athari gani wakati wa utekelezaji. Hilo nalo tunaenda kulifanya na likirudi litaingia kwenye Kamati ya Huduma za Jamii.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Waheshimiwa Wabunge ushauri wenu sana ni muhimu wakati wa utekelezaji wake na kuangalia mambo yote ili wakati wa utekelezaji Wabunge vilevile tusiweze kulaumiwa kule na wananchi. Kwa hiyo, likirudi ushauri wenu unategemewa zaidi ili tuweze kuikamilisha mara moja. (Makofi)