Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 15 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 123 2022-04-29

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BAHATI K. NDINGO K.n.y. MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha Bima za Afya za Wazee ili ziweze kutumika wakiwa nje ya Mikoa ambayo wamepewa Bima hizo.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, wakati Serikali ikiendelea na mchakato wa kukamilisha Muswada wa Bima ya Afya kwa wote, Serikali inaelekeza vituo vyote vya huduma kuwapatia huduma wazee wasio na uwezo waliotimiza vigezo hata wakiwa nje ya maeneo yao. Ahsante. (Makofi)