Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. ALLY Y. MHATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari ya kubebea wagonjwa katika Vituo vitatu vya Afya Wilayani Nanyumbu?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Nashukuru pia kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini pamoja na majibu hayo, kuna vituo vya afya ambavyo viko mbali sana na Hospitali ya Wilaya kiasi ambacho inakuwa shida kwa wagonjwa kupelekwa katika hospitali hiyo. Kwa mfano, Kituo cha Mtambaswala ni kilomita 70 kutoka Hospitali ya Wilaya, Kituo cha Nanyumbu kilomita 40, Kituo cha Michiga kilomita 30; kwa hiyo, kwa umbali huo, naomba kupata commitment ya Serikali kwa sababu kama tutagawa equally kwa Halmashauri zote, kuna vituo vya afya ambavyo vitakuwa havifanyiwi kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, naomba pia kupata majibu ya Serikali: Ni lini Kituo cha Afya cha Mkwedu ambacho kipo katika Jimbo la Newala Vijijini kitapelekewa gari kwa ajili ya wagonjwa kwa sababu kituo kile kinahudumia kata zaidi ya tano?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maimuna Mtanda, Mbunge wa Jimbo la Newala Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Vituo vya Afya vya Mtambaswala, Nanyumbu viko mbali sana kutoka Hospitali ya Halmashauri na Serikali inatambua kwamba vituo vya mbali sana vinahitaji kupata magari ya wagonjwa. Ndiyo maana katika mwaka huu wa fedha Mheshimiwa Rais wetu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ametupa fedha TAMISEMI kwa ajili ya kununua magari 407. Magari ya wagonjwa 195 kwa kila halmashauri na halmashauri hii ya Nanyumbu itapata na magari 212 kwa ajili ya usimamizi wa huduma za afya katika Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, utaona tutakuwa na magari zaidi ya hayo, lakini tutaendelea kutoa kipaumbele kwenye vituo vya mbali zaidi ili vipate magari yakiwemo vituo hivi vya afya.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na Kituo cha Afya cha Mkwedu, naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutatafuta fedha ili tuweze kupeleka gari la wagonjwa. Nafahamu kituo hiki kiko mbali sana na kinahudumia wananchi wengi. Ahsante.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. ALLY Y. MHATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari ya kubebea wagonjwa katika Vituo vitatu vya Afya Wilayani Nanyumbu?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Jimbo la Njombe limekuwa na vituo vitatu vimekamilika muda mrefu sana; na huu mgao wa equal unatupa wasiwasi kwa vile vituo ambavyo vinangojea magari na vimeahidiwa miaka zaidi minne: Je, Serikali itatusaidia kwenye hilo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Mwanyika, Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tunahitaji vituo vyetu viwe na magari ya wagonjwa kila kituo kiwe na gari la wagonjwa. Safari ni hatua. Kwa sasa tunaanza na vituo vile vya kimkakati, lakini mara nyingi uzoefu unaonesha vituo vya afya vingine vinaweza vikawa saved na magari ya wagonjwa yaliyo katika Hospitali za Halmashauri au katika vituo vya afya vya jirani. Kwa hiyo, tutaendelea kuangalia umbali wa kituo cha afya kutoka hospitali na pia population ambayo ina- save ili kuhakikisha kwamba tunapeleka magari katika vituo hivyo. Ahsante. (Makofi)

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. ALLY Y. MHATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari ya kubebea wagonjwa katika Vituo vitatu vya Afya Wilayani Nanyumbu?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Geita ina majimbo mawili na hospitali mbili za wilaya. Sasa kwa maelezo ya Waziri, ina maana likija gari moja itakuwa ni ugomvi ikakae hospitali gani; aidha, likae Jimbo la Geita Vijijini au Busanda, ambapo kila jimbo lina hospitali: Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa special kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuleta magari mawili?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, magari ya wagonjwa yatakayonunuliwa ni magari 195, nasi tuna Halmashauri 184. Kwa hiyo, utaona tuna magari 11 ya ziada na tutaangalia mazingira ambayo tuna ulazima wa kuongeza gari kwenye Halmashauri, tutaongeza. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafanya tathmini kuona magari yaliyopo Geita Vijijini na Mjini na uhitaji na hivyo tunaweza kufanya maamuzi. Kwa hiyo, tutafanya hivyo kwa kadri ya mazingira. Ahsante.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. ALLY Y. MHATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari ya kubebea wagonjwa katika Vituo vitatu vya Afya Wilayani Nanyumbu?

Supplementary Question 4

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itajenga vyumba vya kuhifadhia maiti katika Vituo vya Afya vya Nzihi pamoja na Kiponzero? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jackson Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Kalenga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilishatoa maelekezo ya Halmashauri zote kuanza kwa kutumia mapato ya ndani kwa ujenzi wa miundombinu ambayo iko ndani ya uwezo wao ikiwemo majengo ya kuhifadhia miili ya marehemu kwa maana ya mochwari. Kwa hiyo, naomba Halmashauri ya Wilaya ya Iringa iangalie uwezekano wa kuanza ujenzi wa mochwari kwenye vituo vya afya vya Nzihi na Kiponzero. Pia Serikali tukipata fedha, tutaunga mkono juhudi hizo za Halmashauri. Ahsante. (Makofi)

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. ALLY Y. MHATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari ya kubebea wagonjwa katika Vituo vitatu vya Afya Wilayani Nanyumbu?

Supplementary Question 5

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Halmashauri ya Wilaya ya Same ina majimbo mawili ambayo moja ni la Mashariki na Magharibi na yako mbalimbali sana; lakini Hospitali ya Wilaya iko upande mmoja tu wa magharibi na hata kituo cha afya kilichoko mashariki hakina gari la wagonjwa. Mheshimiwa Waziri, naomba hili aliangalie na aniambie atafanya nini hapa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna baadhi ya vituo vya afya viko mbali sana kutoka Hospitali za Halmashauri ziliko ikiwemo kituo hiki cha afya ambacho Mheshimiwa Mbunge amekitaja. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafanya tathmini na kuona uwezekano wa kupata gari la wagonjwa kwa ajili ya kituo hiki cha afya ili kuweza kusogeza huduma kwa wananchi.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. ALLY Y. MHATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari ya kubebea wagonjwa katika Vituo vitatu vya Afya Wilayani Nanyumbu?

Supplementary Question 6

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba mpaka sasa haina gari hata moja la uhakika la wagonjwa; na ni Halmashari ya Wilaya ambayo imeundwa na majimbo mawili; Jimbo la Kwimba na la Sumve. Mpaka sasa kwenye Jimbo la Sumve hakuna kabisa ambulance: Mheshimiwa Waziri huoni kwamba umefika wakati wa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba yenye majimbo mawili na Halmashauri zote zenye majimbo mawili kugawiwa ambulance kwa kuzingatia kwamba kila Jimbo lipate ambulance yake?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kasalali Mageni Mbunge wa Jimbo la Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nipokee taarifa ya Halmashauri hii ya Kwimba kwamba haina gari la uhakika hata moja la wagonjwa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha wananchi wetu wanapata uhakika wa huduma za rufaa na dharura. Kwa hiyo, tutahakikisha tunapata gari kwa ajili ya Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na kugawa magari mawili kwenye Halmashauri zenye majimbo mawili, tutafanya tathmini kulingana na uhitaji kwa kadri ya vigezo vya kitaalamu na tutaona, ziko Halmashauri zitapata magari zaidi ya moja na pia ziko Halmashauri ambazo zinaweza zikapata gari moja. Ahsante.