Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 15 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 118 2022-04-29

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. ALLY Y. MHATA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka magari ya kubebea wagonjwa katika Vituo vitatu vya Afya Wilayani Nanyumbu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Yahaya Mhata, Mbunge wa Jimbo la Nanyumbu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Nanyumbu ina magari mawili ya kubebea wagonjwa ambayo yanatumika katika Hospitali na Vituo vya Afya. Hata hivyo, magari haya bado ni machache kwa kuzingatia uhitaji uliopo.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO-19 itanunua magari 195 ambapo kila Halmashauri itapata gari la kubebea wagonjwa ikiwemo Halmashauri ya Nanyumbu. Ununuzi huu utaboresha huduma za afya za dharura na rufaa. Ahsante.