Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA K.n.y. MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati miundombinu ya maji katika Kata za Jimbo la Arumeru Mashariki?

Supplementary Question 1

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya wananchi wa Arumeru kwanza kabisa tutoe shukrani kwa majibu mazuri ya Serikali, vilevile kwa niaba ya Mheshimiwa Pallangyo anatoa shukrani nyingi sana kwamba aliomba Shilingi Bilioni 2.7 fedha hizo zimefika na tayari zimeanza kufanya kazi, lakini nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mradi wa maji Kijiji cha Litoho, Kata ya Ukata, unaotokea Liwanga unatoa maji muda wote sijui nisema machafu lakini yasiyokuwa pure yana udongo kwa hiyo yanahitaji ujenzi wa chujio. Je, ni lini Serikali itajenga chujio katika mradi huo.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali kwanza nipende kupokea shukrani kutoka kwa Mbunge wa Arumeru, kwa kweli kupeleka fedha ni wajibu wetu na kipekee tumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa sababu anaendelea kutoa fedha kwenye miradi hii mikubwa ili wananchi waweze kuondokana na matatizo ya maji na kubeba ndoo kichwani.

Mheshimiwa Spika, kwenye ujenzi wa chujio naomba nitoe ahadi kwamba ni moja ya majukumu yetu kama Wizara nimelipokea tutalifanyia kazi. (Makofi)

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA K.n.y. MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati miundombinu ya maji katika Kata za Jimbo la Arumeru Mashariki?

Supplementary Question 2

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, tatizo la chanzo cha maji cha Geita ni kubwa na ningependa kufahamu ni lini Wizara itakarabati ili kuongeza kiwango cha maji kinachozalishwa kwa ajili ya Mji wa Geita.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kanyasu Mbunge wa Geita kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara tumeweka mkakati wa kuona kwamba vyanzo vyote vya maji viweze kutoa maji safi salama na ya kutosha, hivyo hata kwenye Mji wa Geita lipo katika mikakati yetu nipende kumuomba Mheshimiwa Mbunge tuendelee kushirikiana kama ambavyo anafany,a lengo ni kuona wananchi wanaenda kupata maji safi na salama.(Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA K.n.y. MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati miundombinu ya maji katika Kata za Jimbo la Arumeru Mashariki?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kwanza niipongeze Serikali kwa kukamilisha mradi wa maji kutoka Nyamtukuza Wilayani Nyang’wale na sasa hivi maji tumeyapata lakini maji haya si safi na salama kwa sababu mradi ule haukutengenezewa chujio la kuyatibu yale maji.

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga chujio la kutibu maji ili wananchi wasije wakaugua na kupoteza fedha nyingi kwa ajili ya matibabu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hussein Amor Mbunge wa Nyangwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nipokee shukrani zake kwa sababu mradi huu ni ile moja ya miradi vichefuchefu na hapa tunampongeza Mheshimiwa Waziri ameweza kusimamia mradi sasa unatoa maji, suala la chujio ni suala linalofuata katika mwaka ujao wa fedha tutahakikisha na suala la chujio nalo linapewa nafasi.

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA K.n.y. MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati miundombinu ya maji katika Kata za Jimbo la Arumeru Mashariki?

Supplementary Question 4

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza swali moja la nyongeza.

Nilishawahi kuripoti mradi wa Kalumea - Nyehunge Nyakalilo ni kichefuchefu, Mheshimiwa Waziri aliahidi kutembelea mradi ule ili aweze kutoa fundisho kwa watu wanaochezea fedha za Serikali naomba kuuliza tena.

Je, Mheshimiwa Waziri wako tayari kutembelea mradi wa Lumea ili kwenda kutoa fundisho kwa Wakandarasi wanaotumia vibaya fedha za Serikali?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shingongo Mbunge wa Sengerema, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sengerema mimi mwenye nilifika na tuliweza kufanya kazi nzuri na maeneo yale tuliyopita yanakwenda vizuri kwenye mradi huu anaouongelea Mheshimiwa Mbunge mara baada ya Bunge hili tutawasiliana kuona namna gani ya kuweza kufika pale kwa pamoja.

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA K.n.y. MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati miundombinu ya maji katika Kata za Jimbo la Arumeru Mashariki?

Supplementary Question 5

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, katika miradi ya maji ambayo iliyoko katika maeneo yetu tunao mradi mkubwa wa maji eneo la Nyasibu, Mbungo, Ngoma ambao na wenyewe umekaa kwa muda mrefu nini majibu ya Serikali ili mradi huo uanze kama ulivyopangwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Tabasamu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mradi huu wa Nyasibu tayari tumeshawaagiza vijana wetu waweze kuona namna ya kuweza kuuendeleza Mheshimiwa Mbunge baada ya hapa tuonane tuweke vizuri ili suala kwa sababu huu mradi ni muhimu wote tunafahamu.