Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 13 Water and Irrigation Wizara ya Maji 102 2022-04-27

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA K.n.y. MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati miundombinu ya maji katika Kata za Jimbo la Arumeru Mashariki?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Arumeru hali ya huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama ni asilimia 71.5 huduma hii inapatikana kutoka kwenye skimu 39 zilizojengwa kabla ya mwaka 2000. Katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imeendelea na ukarabati wa miundombinu ya miradi ya maji kwenye skimu za Kikwe-Msitu wa Mbogo, Kata ya Kikwe na Mbuguni Olkungabo - Ngabobo (Kata ya Ngarenanyuki na Ngabobo na Ngurdoto-Sakila - Ngyeku Kata za Imbaseni, Maji ya Chai na Kikatiti. Kazi hii itakamilika Mwezi Juni, 2022. Aidha, katika kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji, miradi mipya itajengwa kwa ajili ya kutoa huduma kwenye Kata za Nkoarisambu na Akheri ambapo kazi hii itakamilika Septemba, 2022.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2022/ 2023, ukarabati wa miundombinu ya maji utaendelea ili kuhakikisha huduma ya upatikanaji wa maji katika Kata zote inakuwa endelevu.