Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani kuirejeshea Halmashauri ya Liwale fedha za kutekeleza miradi ya kimkakati iliyorudishwa Hazina ili iweze kujenga Stendi ya Kisasa?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru Serikali kwa kuonesha commitment ya kutaka kujenga stendi hii ya kisasa, lakini nimewasiliana na watu wa Halmashauri, wanasema kwamba kwa upande wa Halmashauri mchakato umeshakamilika kutoka kwenye ngazi ya Wilaya mpaka kwenye ngazi ya Mkoa. Sasa hivi Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kuwasiliana na watu wa TAMISEMI kwa kuona kwamba mradi huu umekwama kwenye ngazi hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa sababu kumebakizwa miezi miwili bajeti aliyoitaja hapo inakwenda kukamilika. Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kututengea tena fedha kwenye bajeti hii iwapo kama fedha zile za mwanzo zitakuwa bado hazijatumika? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kabla ya kujibu maswali hayo naomba nimpongeze sana Kaka yangu Kuchauka kwa kazi nzuri anayoifanya katika Jimbo la Liwale.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha na Mipango ipo tayari kuwasiliana na Wizara ya TAMISEMI nachukua nafasi hii nitoe maelekezo kwa wataalam wetu kufanya mawasiliano ya haraka sana kuona hadhi ya project hii imefikia wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la pili kwa kuwa Serikali ina nia njema ya kujenga stendi ya kisasa, basi kama haikukamilika mwaka wa 2021/2022 basi bajeti inayokuja tutatenga tena fedha hiyo ili kusudi tuone mradi huo umekamilika. Ahsante. (Makofi)