Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 11 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 96 2022-04-22

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani kuirejeshea Halmashauri ya Liwale fedha za kutekeleza miradi ya kimkakati iliyorudishwa Hazina ili iweze kujenga Stendi ya Kisasa?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa stendi ya kisasa ya Liwale ni moja kati ya miradi ya kimkakati ya kuongeza mapato kwa Halmashauri, ambapo mwaka 2018 Serikali iliingia mkataba na Halmashauri ya Wilaya ya Liwale Mkoani Lindi kutekeleza mradi huo kwa gharama ya Shilingi Bilioni 1.2.

Mheshimiwa Spika, nia ya Serikali ni kuhakikisha kuwa mradi huu unatekelezwa. Hivyo, kutokana na umuhimu wa mradi huu, katika mwaka 2021/2022 Halmashauri ya Wilaya ya Liwale imetengewa Shilingi Bilioni Moja kwa ajili ya ujenzi wa stendi ya kisasa ya Liwale. Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Liwale kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI inahimizwa kukamilisha taratibu za maombi ya fedha na kuwasilisha Wizara ya Fedha na Mipango. Ahsante.