Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Korogwe – Dindira – Bumbuli hadi Soni ambayo ilitengewa fedha kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi katika mwaka wa fedha 2020/2021?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kama tutakwenda na majibu haya mpaka wakati wa bajeti, hali itakuwa tete hapa. Pamoja na hayo naomba kuuliza swali mawili ya nyongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kwamba upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umekuwa ukifanyika kwa awamu na tayari kipande cha kwanza kimekamilika na kipande cha pili kiko asilimia 81. Serikali haioni sasa ni vizuri kuanza pia ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami, kwa awamu kwa vipande tukianza na bajeti inayokuja mwaka 2022/2023?

Mheshimiwa Spika, Pamoja na ahadi hizo za barabara ya lami, Serikali imekuwa ikijitahidi kutenga fedha kwa ajili ya matengenezo na ukarabati wa barabara hii pamoja na barabara ile ya Korogwe - Magoma kwenda mpaka Maramba. Lakini matengenezo yamekuwa yamekuwa yakifanyika kwa kuchelewa sana lakini pia kifusi kinachowekwa kinakuwa hakina ubora unaoendena na mazingira tuliyokuwa nayo. Na hivi tunavyoongea sasa hivi barabara ya kwa Shemshi haipitiki kwa sababu vifusi havijasambazwa; ni nini kauli ya Serikali juu ya wakandarasi hawa wanaofanya kazi chini ya kiwango na kuwasababishia wananchi wetu matatizo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFRY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inafanya usanifu wa kina wa barabara hii yote aliyoainisha Mheshimiwa Mbunge, ya kutoka Soni, Bumbuli, Dindira hadi Korogwe ili gharama halisi iweze kufanyika na tuone kama kutakuwa na ulazima wa kuwa na loti moja ama mbili. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa tukishakamilisha usanifu wa hiyo barabara tuona namna ya kuanza kuijenga hiyo barabara; na ni azma ya Serikali kuijenga barabara yote hii kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, na kuhusu barabara aliyoitaja ya pili, ambayo inaanzia Korogwe, Bombo Mtoni, Maramba hadi Mabokweni, barabara hii inapita kwenye sehemu nyingi ya miinuko. Kwa kawaida arabara kwa kawaida nyingi ambazo zinapita kwenye miinuko zinaoshwa na mvua, tumewaagiza mameneja, wa mikoa waweze kuainisha maeneo yote korofi, ili tutafute namna ya kudhibiti maeneo yote yaliyo bondeni na kwenye miinuko ili tuweze kutafuta utaratibu muhimu wa kuweza kudhibiti hayo maeneo ikiwa ni pamoja na kuweka lami nyepesi ama zege ama strip za mawe ambazo tunahakika barabara hizi zitakuwa na uwezo wa kuitika kwa muda mrefu bila kuitika.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Korogwe – Dindira – Bumbuli hadi Soni ambayo ilitengewa fedha kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi katika mwaka wa fedha 2020/2021?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa swali la nyongeza, naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri barabara ya kutoka Tambuka Reli, Nyagulugulu mpaka Mahina ni lini Serikali itaanza kuijenga kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFRY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stanslaus Mabula, Mbunge wa Nyamagana kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeza Mheshimiwa Mabula, amekuwa akija ofisini kuhusu barabara hii. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Nyamagana kwamba Serikali inakamilisha usanifu wa kina wa barabara hii na ina mpango wa kuanza kuijenga barabara hii kwa haraka sana kwa kiwango cha lami kwa sababu kwa watu ambao wamefika Mwanza, ndio barabara pekee ambayo inapotokea changamoto yoyote kati ya Mkuyuni, Igogo kwenda mjini ndiyo inaweza kuwa ni bypass kwa ajili ya watu kufika mjini.

Mheshimiwa Spika kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mpango wa Serikali ni kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami haraka inavyowezekana.