Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 11 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 93 2022-04-22

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Korogwe – Dindira – Bumbuli hadi Soni ambayo ilitengewa fedha kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi katika mwaka wa fedha 2020/2021?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFRY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, upembuzi yakinifu na Usanifu wa Kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami Barabara ya Korogwe – Dindira – Bumbuli – Soni (km 77) unafanyika kwa awamu. Sehemu ya kutoka Soni hadi Bumbuli (km 21.7) upembuzi yakinifu na usanifu wa Kina umekamilika. Kwa Sehemu iliyobaki ya kutoka Bumbuli hadi Korogwe (km 55.3), kazi ya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina inaendelea na imefikia asilimia 81.

Mheshimiwa Spika, baada ya Kazi ya Upembuzi Upembuzi yakinifu na Usanifu wa Kina kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami.