Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga majosho ya mifugo katika Kata za Makilawa, Igelansoni, Iyumbu, Ighombwe, Mgungira na Mwaru Wilayani Ikungi?

Supplementary Question 1

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nataka nijue sasa commitment ya Serikali kwa Kata zilizobaki, kwa maana katika majibu ya msingi inaonesha kwamba kuna Kata moja tu imejengewa majosho na Jimbo la Singida Magharibi ni moja ya Majimbo ambayo yana wafugaji wengi sana: -

Je, Serikali lini itakwenda kutekeleza ujenzi wa majosho katika Kata za Igelansoni, Makilawa, Mwaru, Igombwe pamoja na Minyuge?

Swali la pili: Je, Waziri yuko tayari kuongozana nami Mbunge akajionee namna wafugaji wanapata adha kulingana na changamoto ya magonjwa katika mifugo yao kutokana na kutokuwepo kwa majosho?

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Elibariki Kingu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, natambua ya kwamba uhitaji wa majosho nchini ni mkubwa na kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi tumeelekezwa kuweka josho kwenye kila Kijiji kilicho na mifugo. Kwa hiyo, kwenye mpango wetu wa Wizara, mwaka huu fedha tutakaouanza tumeweka pia mpango wa kuendelea kujenga majosho kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini. Sasa tutatoa kipaumbele kwenye maeneo aliyoyataja Mheshimiwa Kingu; Gelansoni, Iyumbu, Igombwe na maeneo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, juu ya suala la kuambatana naye ili twende kukutana na wafugaji wake. Niko tayari kufanya hivyo na pengine kama tutapata wakati, weekend mojawapo tunaweza kuambatana ili tukutane na hao wafugaji.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga majosho ya mifugo katika Kata za Makilawa, Igelansoni, Iyumbu, Ighombwe, Mgungira na Mwaru Wilayani Ikungi?

Supplementary Question 2

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, kwenye Jimbo la Kibaha Vijijini kwenye Kata ya Magindu, Ruvu, Gwata na Dutumi kuna wafugaji wa kutosha lakini majosho hakuna: Je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kunipatia sehemu ya majosho aliyoyataja kwamba yapo kwenye bajeti? (Makofi)

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwakamo, Mbunge wa Kibaha kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tutapanga vizuri kwenye majosho ambayo Serikali itatupa fedha kwa mwaka wa fedha ujao ili kuhakikisha kwamba Jimbo la Kibaha pia linapata majosho, yanaweza yasiwe yote lakini angalau maeneo yaliyo muhimu yenye wafugaji wengi, tutaongea pamoja na Mheshimiwa Mbunge ili tuone kwamba maeneo hayo yanapata majosho pia.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga majosho ya mifugo katika Kata za Makilawa, Igelansoni, Iyumbu, Ighombwe, Mgungira na Mwaru Wilayani Ikungi?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Tatizo la majosho lipo maeneo mengi. Halmashauri ya Mji wa Bunda, nadhani mjomba unajua kuna wafugaji wengi, lakini kuna malambo ambayo hayako kwenye hali nzuri; Kinyambwiga, Gushigwamara, Kisangwa pamoja na Rwabu: Ni lini mtayakarabati hayo malambo ili wananchi wa Bunda waweze kupata huduma ya kulishia mifugo yao?

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nilishafika Bunda, nilishayaona hayo malambo, tulishaenda na Mheshimiwa Getere tukazunguka tukaona maeneo ya malambo ambayo yameharibika. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwenye mwaka ujao 2023 tuna mpango wa kukarabati malambo mengi kidogo. Pia tuna mpango wa kujenga malambo mapya, yatakuwa mengi, zaidi ya manne ambayo mlitupa bajeti ya mwaka huu. Kwa hiyo, tutafikiria kuangalia wananchi na wafugaji wa Bunda ili tuone malambo yao ambayo yameharibika ni kwa namna gani tutaweza kuyakarabati.

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga majosho ya mifugo katika Kata za Makilawa, Igelansoni, Iyumbu, Ighombwe, Mgungira na Mwaru Wilayani Ikungi?

Supplementary Question 4

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Changamoto ya majosho iliyopo kwenye Singida Magharibi ni sawa na changamoto iliyopo kwenye Jimbo la Igunga, kwenye Kata ya Kinikinila, Isakamaliwa, Mamashimba, Kilungu pamoja na Igulubi: -

Je, ni lini Wizara itatatua changamoto hii, ukizingatia Jimbo la Igunga ni miongoni mwa majimbo yenye mifugo mingi nchini?

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nicholaus Ngassa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Igunga na Wilaya ya Igunga kwa ujumla tulipangia mwaka huu wa fedha kwamba tungeweza kujenga majosho zaidi ya matano, lakini majosho matatu hatukuweza kuyajenga kwa sababu hatukupata ushirikiano mzuri na Ofisi ya Mkurugenzi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ninaamini kwenye bajeti ijayo, kwa sababu pia tumetenga majosho kwa Wilaya ya Igunga, tutapata ushirikiano wa kutosha na kwa hivyo maeneo aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge tutayapangia kujenga majosho. Tupate ushirikiano wa kutosha ili kwamba majosho yatakayopangwa kwa wilaya hiyo basi yaweze kukamilishwa.

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga majosho ya mifugo katika Kata za Makilawa, Igelansoni, Iyumbu, Ighombwe, Mgungira na Mwaru Wilayani Ikungi?

Supplementary Question 5

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Jimbo la Singida Mashariki ni miongoni mwa majimbo yenye wafugaji wengi sana, na Mheshimiwa Waziri alishawahi kuniahidi majosho takribani matatu kwenye Kata za Siuyu, Ulyapiti, pamoja na Isuna.

Sasa ni nini kauli yake kwa mwaka huu wa fedha?

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, namtafutia majibu.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga majosho ya mifugo katika Kata za Makilawa, Igelansoni, Iyumbu, Ighombwe, Mgungira na Mwaru Wilayani Ikungi?

Supplementary Question 6

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Vijiji vya Ombiri, Muungano, Golopaguma, Dalayi navyo vina matatizo makubwa ya majosho kwa ajili ya mifugo. Na ikumbukwe kwa Mkoa wa Dodoma Wilaya ya Chemba ndiyo yenye mifugo mingi. Naomba kujua commitment ya Serikali sasa ni lini tutaenda kujenga majosho kwenye vijiji hivyo? Ahsante sana.

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa Wilaya na Mkoa wa Dodoma kwa ujumla una mifugo mingi sana. Kwa mwaka huu wa fedha tunaoenda nao angalau kila wilaya tulikuwa tumewapangia majosho si chini ya manne, tuliwapa upendeleo kidogo. Sasa safari ijayo tutaangalia pia hasa kwa Jimbo la Mheshimiwa Mbunge wa Chemba, tuone ni kwa namna gani tunaweza kupanga kujenga majosho mengine ili Mheshimiwa Mbunge na wafugaji wake waweze pia kufaidika.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga majosho ya mifugo katika Kata za Makilawa, Igelansoni, Iyumbu, Ighombwe, Mgungira na Mwaru Wilayani Ikungi?

Supplementary Question 7

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa hadi leo ni mwaka wa kumi na mbili niko Bungeni na sijawahi kutembelewa na Waziri wa Mifugo katika jimbo langu, je, Waziri atakuwa yuko tayari kutembelea jimbo langu kuja kuongea na wafugaji ikiwemo na changamoto hizo za majosho na mambo mengine?

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Nyanghwale, Mbunge ambaye pia ana wafugaji wengi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, niko tayari kumtembelea Mheshimiwa Mbunge na jimbo lake. Najua wapo wafugaji wengi na kwa hiyo kumkosa Waziri wa Mifugo au msaidizi wake itakuwa ni tatizo. Sasa niko tayari kufanya hivyo kipindi hiki cha bunge tunaweza kutafuta wikiendi mojawapo twende au baada ya Bunge ili ya kwamba tuweze kukutana na wafugaji wake tutatue matatizo na changamoto zilizoko zinazohusiana na mifugo.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga majosho ya mifugo katika Kata za Makilawa, Igelansoni, Iyumbu, Ighombwe, Mgungira na Mwaru Wilayani Ikungi?

Supplementary Question 8

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa, naomba niulize swali moja la nyongeza. Mheshimiwa Waziri ulipokuja kutembelea mnada wa Hororo, mojawapo ya changomoto tuliyoizungumza ni ukarabati wa lambo la Ng’ombeni. Je, ahadi iko pale pale, kwamba litakarabatiwa?

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kitandula kama ifuatavyo: -

Ahadi yetu Mheshimiwa Mbunge iko pale pale, na tutafanya hiyo kazi mpaka ikamilike ikiwa ni pamoja na kukamilisha ujenzi wa mnada huo. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge kuwa na uhakika kwamba sisi kazi hiyo tulishaanza kuifanya na kwa hivyo tutaikamilisha kama ambavyo tumepanga. Ahsante sana.