Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kutatua changamoto zinazokabili Miradi ya Umwagiliaji ya Mkoga na Kitwiru iliyopo Manispaa ya Iringa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali madogo mawili. Kwanza nashukuru kwa majibu ya Serikali. Kilimo cha uhakika ni kilimo cha umwagiliaji. Napenda kufahamu hatua iliyofikiwa kwa utekelezaji wa miradi ya Mgombilenga iliyopo Kata ya Kitwiru na Mradi wa UNI wa Kata ya Nyanzwa, kwa sababu hii miradi, Wabunge wa Iringa ni muda mrefu sana tumekuwa tukiifuatilia.

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, katika Wilaya ya Mufindi Kaskazini tuna skimu ya Igoma, Kata ya Sadani na Ikwea. Hii miradi kwa mfano hii ya Ikweha ililetewa shilingi milioni 800, lakini utekelezaji wake mpaka sasa hivi bado haujaweza kueleweka. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri atujibu, Mkoa wetu wa Iringa ni wa kilimo. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Ritta Enespher Kabati, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu miradi ya Mgombilenga na Nyanzwa iliyopo Wilaya ya Kilolo, katika bajeti ya mwaka 2022/2023 Serikali itakwenda kuikabarati miradi hii na kuitekeleza. Hivyo nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la pili la mradi wa Ikweha, ni kweli pale tuna mradi ambao mpaka hivi sasa umeshatumia shilingi milioni 800 ambazo zimetokana na fedha za DADPs pamoja na DIDF. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tunafahamu changamoto iliyoko pale, hivi sasa Serikali tunatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa bwawa. Vile vile mimi mwenyewe nitakwenda kutembelea mradi huu ili kutatua baadhi ya changamoto zilizopo pale na kuwafanya wakulima wawe na amani na kufanya kilimo cha umwangiliaji katika eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, namwahidi tu Mheshimiwa Mbunge, kama Serikali, tunafahamu changamoto iliyopo pale na tunatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa bwawa.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kutatua changamoto zinazokabili Miradi ya Umwagiliaji ya Mkoga na Kitwiru iliyopo Manispaa ya Iringa?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, Mradi wa Umwagiliaji wa Izazi uliyopo Jimbo la Isimani una changamoto ya uchakavu wa miundombinu pia. Ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kukarabati miundombinu hiyo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mirada yote ya umwagiliaji tuliyonayo hapa nchini hivi sasa tumeweka mpango mkakati katika mwaka wa fedha ujao kuhakikisha kwamba Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, inaipitia miradi yote nchini Tanzania, tufanye uhakiki, tujue miradi gani inafanya kazi, ipi haifanyi kazi na ipi inahitaji marekebisho ya kiwango gani?

Mheshimiwa Spika, katika uhakiki huo pia tutagusa na miradi ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kutatua changamoto zinazokabili Miradi ya Umwagiliaji ya Mkoga na Kitwiru iliyopo Manispaa ya Iringa?

Supplementary Question 3

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Sisi tuna mradi wa Skimu ya Shitage, iligharimu fedha nyingi sana, haifanyi kazi. Lini ahadi ya Mheshimiwa Waziri ya kutengenezwa hiyo skimu itatekelezwa ili wananchi wapate faida ya mradi ule?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Almas Maige, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema pale awali, tunafahamu kwamba kilimo cha umwagiliaji ndicho kilimo hasa ambacho kitamkumboa mkulima wa Tanzania. Kwa umuhimu huo, tumeamua kwa dhati kabisa kuipitia hii miradi yote ikiwemo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameisema. Nimwondoe hofu ya kwamba tumejipanga kuhakikisha miradi hii inafanya kazi.

Kwa hiyo, katika eneo lake pia tutapita na hivi sasa tunaendelea kutafuta fedha na mtaona kwenye bajeti yetu inayokuja, nguvu kubwa hivi sasa imewekwa kwenye Tume ya Umwagiliaji kuwawezesha ili tuweze kufanya kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kutatua changamoto zinazokabili Miradi ya Umwagiliaji ya Mkoga na Kitwiru iliyopo Manispaa ya Iringa?

Supplementary Question 4

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Jimbo la Mwibara ni kama limezungukwa na maji, lakini hatuna hata mradi mmoja wa umwagiliaji maji: Je, ni lini Serikali itajenga miradi hiyo katika Kata ya Namuhula, Igundu, Iramba na Kasuguti? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Charles Kajege, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ni jambo ambalo ameliwasilisha hapa, nami nitaelekeza wataalam wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wakalitembelee eneo hilo na baada ya hapo waone namna ya kuwasaidia wananchi katika eneo hilo kufanya kilimo cha umwagiliaji.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kutatua changamoto zinazokabili Miradi ya Umwagiliaji ya Mkoga na Kitwiru iliyopo Manispaa ya Iringa?

Supplementary Question 5

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Pale Ruaha Mbuyuni kuna mradi wa umwagiliaji ulikarabatiwa na Wizara kwa force account, lakini sasa mto ule umeanza kuchepuka tena: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari tuongozane ili tuweze kuangalia tunafanyaje katika kuukarabati?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Justin Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, namwahidi tu kwamba Mheshimiwa Mbunge, kabla mimi na yeye hatujaongozana Jumatatu, Afisa wetu wa Tume ya Umwagiliaji walioko pale Iringa atakwenda kuukagua kwanza na kutupa taarifa, nami na yeye pia tutakwenda pamoja.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kutatua changamoto zinazokabili Miradi ya Umwagiliaji ya Mkoga na Kitwiru iliyopo Manispaa ya Iringa?

Supplementary Question 6

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Jimbo la Tunduru Kusini kuna miradi miwili ambayo ilifanyiwa kazi na imechukua hela nyingi zaidi ya shilingi bilioni tatu kutengenezwa pamoja na barabara, lakini miradi ile haifanyi kazi. Je, Serikali inampango gani wa kuweza kukamilisha miradi ile, mradi wa Mishaji pamoja na mradi wa Madaba, uliopo Azimio?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daimu Mpakate, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika majibu yangu ya awali, tumejipanga kuhakikisha miradi yote hii inafanya kazi. Hivyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba katika uhakiki ambao tutaufanya, tutapitia pamoja na maeneo yake ili kuona miradi hii changamoto yake ni nini; na mwisho wa siku tuweze kuikwamua na wananchi waweze kufanya kilimo cha umwagiliaji.