Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 11 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 89 2022-04-22

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kutatua changamoto zinazokabili Miradi ya Umwagiliaji ya Mkoga na Kitwiru iliyopo Manispaa ya Iringa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Enespher Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Miradi ya umwagiliaji ya Cherehani Mkoga yenye hekta 750 na Kitwiru yenye hekta 100 iliyopo katika Manispaa ya Iringa inakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo uchakavu wa miundombinu ya umwagiliaji iliyojengwa muda mrefu; kutokamilika kwa miundombinu, pamoja na miundombinu kuharibiwa na mafuriko.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Umwagiliaji inaendelea kutafuta fedha kutoka kwa wadau wa maendeleo kwa ajili ya kukamilisha miradi ya umwagiliaji mbalimbali ikiwemo miradi ya Mkoga na Kitwiru.