Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaiongezea TARURA fedha ili iweze kuzihudumia barabara za Wilaya ya Kyerwa?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Jiografia ya Jimbo la Kyerwa ni milima na mabonde, hivyo kuhitaji madaraja na barabara kwa maana maeneo mengi hayapitiki. Bajeti ya bilioni mbili haitoshi, nataka kujua commitment ya Serikali ni kwa kiwango gani itaongeza bajeti ili kuweza kusababisha maeneo mengi yafikike?

Mheshimiwa Spika, swali la pili barabara ya Nkwenda- Kakanza-Kimuli mpaka Mabira inatumika na kata zaidi ya 5 na kwa TARURA wamepewa scope ya kilometa tatu ambayo ina urefu wa zaidi ya kilometa 30. Je, ni sahihi kweli kutoa kiwango hiki cha fedha kwa barabara hii nataka kujua mkakati wa dharura kupeleka fedha?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anatropia Lwehikira Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kumpongeza Mheshimiwa Anatropia kwa namna ambavyo anashirikiana na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kyerwa Mheshimiwa Innocent Bilakwate na hoja hizi zote ambazo Mheshimiwa Mbunge amezileta Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo amekuwa mara kwa mara anazileta, kwa hiyo niwapongeze kwa ushirikiano huo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na fedha kwa maana za madaraja, hali ya milima na mabonde na hali ya mvua tunafahamu na ndio maana Serikali imeendelea kuongeza fedha kutoka bilioni moja mpaka bilioni mbili na milioni mia nane na tisini katika Wilaya ya Kyerwa ili kuhakikisha inaendelea kujenga madaraja, makalveti na barabara. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali itaendelea kuweka jitihada hizo.

Mheshimiwa Spika, hii barabara ambayo inahudumia kata nyingi na inahitaji fedha zaidi ndio maana Serikali imeongeza bajeti na tutaendelea kuongeza bajeti ili tuhakikishe tunafikia kilometa zote 30 ili kata zote ziweze kunufaika. Ahsante sana.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaiongezea TARURA fedha ili iweze kuzihudumia barabara za Wilaya ya Kyerwa?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Barabara za Wilaya ya Ileje zinakabiliwa na changamoto kubwa sana ya kutopitika hasa wakati wa masika. Naomba kufahamu ni lini Serikali itaipatia fedha TARURA Wilaya ya Ileje ili kuwaondolea adha wananchi wa Wilaya ya Ileje? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka huu wa fedha, moja ya halmashauri ambazo zimeongezewa bajeti ili kuweza kukidhi matengenezo ya barabara za vijijini na mijini ni Halmashauri ya Wilaya ya Ileje. Hivyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, hiyo barabara ambayo ameitaja ni sehemu ya bajeti ya mwaka ujao wa fedha na tutahakikisha kwamba tunaendelea kuitengeneza kwa awamu ili iweze kupitika vizuri. Ahsante.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaiongezea TARURA fedha ili iweze kuzihudumia barabara za Wilaya ya Kyerwa?

Supplementary Question 3

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na Serikali kuongeza bajeti kwa Wilaya ya Kyerwa, lakini tulileta ombi maalum kwa ajili ya barabara ya Kibingo kwenda Rwesinga, Barabara ya Mabira kwenda Nyamiri- Makamuri, barabara ya Kikukuru -Mkunyu - Lwele, barabara ya Kakanya - Lwele pamoja Bushongore. Ombi hili ni lini litatekelezwa ili kuondoa changamoto iliyopo Kyerwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, Mbunge wa Jimbo la Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Bilakwate kwa namna ambavyo anaendelea kuwapambania wananchi wa Jimbo la Kyerwa.

Mheshimiwa Spika, pia nimhakikishie ni kweli ameleta maombi maalum ya barabara zenye urefu wa takribani kilomita 55 ambazo amezitaja. Tayari Ofisi ya Rais, TAMISEMi tumepokea na tutaanza utekelezaji mwaka ujao wa fedha kuhakikisha barabara zote zinapitika vizuri. Ahsante.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaiongezea TARURA fedha ili iweze kuzihudumia barabara za Wilaya ya Kyerwa?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Je, ni kwa nini Serikali isipeleke pesa za miradi hii ya TARURA kwa meneja wa wilaya badala ya mkoa ambako mara nyingi zimekuwa zinasababisha urasimu kwenye utekelezaji wa miradi hii ya barabara zilizo chini ya TARURA?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba fedha za matengenezo ya barabara zimekuwa zikipelekwa katika ngazi ya mikoa na siyo ngazi ya Mameneja wa Wilaya na sababu ya msingi ilikuwa muundo wa TARURA uliweka watendaji wengi zaidi kwenye ngazi ya mkoa kwa maana ya wataalam; Wahasibu, wataalam wa manunuzi na wengine. Kwa hiyo ilikuwa ni vyema sana kupeleka fedha kwenye ngazi ya mkoa ambayo ina watendaji wengi kuliko halmashauri. Utaratibu huu tunaendelea kuutekeleza, lakini pale tutakapoona tuna sababu ya kupitia upya tutafanya hivyo.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaiongezea TARURA fedha ili iweze kuzihudumia barabara za Wilaya ya Kyerwa?

Supplementary Question 5

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Barabara ya Katesi - Iteka inaunganishwa na daraja muhimu katika Mto Mpanda, kwa bahati mbaya daraja hilo limekatika. Je, ni lini Serikali itaongezea fedha TARURA ili walitengeneze daraja hilo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sebastian Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda pia ni moja ya halmashauri ambazo zimeongezewa bajeti ya barabara. Lakini nimhakikishie kwamba mpango wa Serikali ni kuainisha na tayari nimeshainisha madaraja korofi yote na makalvati ili kuhakikisha tunaongeza fedha za ujenzi wa madaraja hayo yaweze kupitika. Hivyo nawaelekeza TARURA, Mkoa wa Katavi na Manispaa ya Mpanda wahakikishe wanaleta andiko la daraja hili ili TAMISEMI tuweze kuona namna ya kutafuta fedha kwenda kufanya ujenzi wa daraja hilo. Ahsante.

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaiongezea TARURA fedha ili iweze kuzihudumia barabara za Wilaya ya Kyerwa?

Supplementary Question 6

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Kibiti tumepatiwa fedha shilingi bilioni 6.2, tumejenga daraja zuri sana pale Mbochi ambalo linaunganisha wananchi wa Mbwela na Mbochi na kuja Kibiti Mjini. Hata hivyo, kuna kipande cha kilometa 35 ambacho ikinyesha mvua kinakuwa kipo katika hali mbaya sana.

Je, ni nini tamko la Serikali ili kuweza kuhakikisha kwamba tunakwenda kutengeneza kipande kilichobaki?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Twaha Mpembenwe, Mbunge wa Jimbo la Kibiti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na tuendelee kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan kwa fedha nyingi sana ambazo amezileta katika majimbo yetu ikiwepo Jimbo la Kibiti. Nimhakikishie kipande cha kilomita tatu ni kipaumbele kwa sababu kama tumepeleka billions za fedha katika daraja lazima tukamilishe kilomita tatu ili hilo daraja liweze kuwa na tija. Kwa hiyo namhakikishia kwamba tutatafuta fedha kuhakikisha kilomita hizi tatu zinatengenezwa ahsante.

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaiongezea TARURA fedha ili iweze kuzihudumia barabara za Wilaya ya Kyerwa?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipatia fursa hii ya kuuliza swali la nyongeza. Mazingira ya Kyerwa na Muleba yanafanana kutokana na mvua nyingi, milima na mabonde. Tuna barabara nyingi ambazo hazipitiki hasa kipindi cha mvua. Tulileta ombi letu kwa ajili ya barabara ya Kimea Burigi na Luhanga- Kiholele. Je, ni lini Serikali itatupatia pesa kwa ajili ya kutengeneza hizo barabara?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oscar Kikoyo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba jimbo hili pia lina changamoto ya milima, mabonde na linahitaji kupata fedha za kutosha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hizi na ni kweli kwamba Mheshimiwa Mbunge alileta ombi maalum. Nimhakikishie kwamba maombi maalum yote yaliyoletwa yanafanyiwa tathmini na Ofisi ya Rais, TAMISEMI kupitia TARURA na tutahakikisha yanatafutiwa fedha ili yaweze kufanyiwa kazi. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge nimhakikishie kwamba tutalipa kipaumbele pia eneo ambalo wameomba maombi maalum. Ahsante.