Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 87 2022-04-22

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaiongezea TARURA fedha ili iweze kuzihudumia barabara za Wilaya ya Kyerwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Lwehikira Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kyerwa ni Wilaya ambayo kwa jiografia ina milima, miteremko pamoja baadhi ya barabara kupita katika maeneo yenye ardhi oevu. Serikali imekuwa ikitenga fedha kila mwaka kwa ajili ya matengenezo ya barabara na madaraja.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeongeza bajeti ya kuboresha miundombinu ya barabara katika Wilaya ya Kyerwa kutoka Shilingi bilioni 1.39 katika mwaka wa fedha 2020/2021 hadi Shilingi bilioni 2.89. Ongezeko hili linatokana na Serikali kuongeza vyanzo vingine ambavyo ni tozo ya mafuta Shilingi bilioni 1.00, Mfuko Mkuu wa Serikali Shilingi milioni 500.00 na Mfuko wa Barabara Shilingi bilioni 1.39.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuongeza wigo wa matengenezo ya barabara pamoja na kufungua barabara mpya katika Wilaya ya Kyerwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Ahsante.