Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzalisha Mbegu bora za Parachichi aina ya Hass na kuzigawa kwa wakulima kwa bei nafuu?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa nimekuwa nikifuatilia sana mbegu za parachichi katika Bunge hili kwa kipindi kirefu; na kwa kuwa leo nimeambiwa itazalishwa miche milioni 20 ya ruzuku; na kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro ikiwemo Siha, Hai, Rombo, Mwanga, Same na Moshi Vijijini, wote wanasubiri miche hiyo kwa hamu, naomba kujua, mgao wetu ni miche mingapi kwa hii awamu itakayotoka? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa parachichi lina wadau wengi sana, naomba pia kufahamu, Serikali imejiunganishaje na wadau hao ili kupata soko la uhakika la parachichi ambalo ni perishable, kwa kipindi hicho ambacho kipo na kinachoendelea katika soko la nje na ndani? Naomba kufahamu. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shally Josepha Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa namna anavyowapigania wakulima wa parachichi katika Mkoa wa Kilimanjaro. Katika maswali yake; la kwanza, mgao utatokana na mahitaji. Siyo rahisi sana kutamka hapa Bungeni kwamba nitapeleka miche mingapi katika Mkoa wa Kilimanjaro, lakini mahitaji yataamua miche mingapi iende katika Mkoa wa Kilimanjaro. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge avute Subira, tukianza zoezi hili, najua tutakuwa pamoja, yale mahitaji ya wakulima Mkoa wa Kilimanjaro tutahakikisha kwamba tunayafikia ili wakulima waendelee kulima kwa tija. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili kuhusu soko la uhakika, katika eneo ambalo tumelifanyia kazi la utafutaji wa masoko katika mazao yetu ni pamoja na parachichi. Hivi sasa tarehe 25 Novemba, 2011 Mamlaka ya Afya ya Mimea India walitupatia kibali cha kupeleka parachichi India, na hivi sasa wakulima wetu wameanza kupeleka parachichi India. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile tunauza parachichi yetu Afrika ya Kusini. Pia tunakamilisha mazungumzo na China juu ya phytol-sanitary, tutaanza pia kupeleka parachichi yetu pia China. Hivi sasa ninavyozungumza, wazalishaji wetu wadogo wadogo wameshapata masoko ya uhakika kule Hispania na Marekani pia.

Mheshimiwa Spika, kuhusu masuala ya soko, soko la uhakika lipo, isipokuwa tulikuwa tuna changamoto moja ambayo tumeshai-address hivi sasa, ilikuwa ni lazima zao letu li-meet international standard, na hivi sasa tunayo maabara yetu pale Arusha ambayo tumeiboresha na hivi sasa tumepata accreditation ambayo ni namba 17025. Kwa hiyo, zao lolote ambalo linatoka Tanzania hivi sasa lina uhakika soko nje ya mipaka ya Tanzania. (Makofi)

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzalisha Mbegu bora za Parachichi aina ya Hass na kuzigawa kwa wakulima kwa bei nafuu?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuniona niulize swali dogo la nyongeza. Pamoja na kugawa mbegu bure ambapo tunashukuru, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba wananchi hasa wakulima wadogo wadogo wanapata utaalam hasa kwenye maeneo ya dawa na magonjwa yanayoshambulia zao hili la parachichi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deodatus Mwanyika kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema pale awali katika majibu yangu ya msingi, zao la parachichi ambalo ni dhahabu ya kijani tunalipa kipaumbele kikubwa na tunakuja na mkakati madhubuti wa kuhakikisha tunawasaidia wakulima wetu kuanzia huduma za ugani mpaka upatikanaji wa pembejeo na waweze kuzalisha kwa tija. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba ni zao ambalo tunalipa kipaumbele na tutahakikisha kwamba wakulima wetu wanapata elimu ya kutosha na kanuni bora za kilimo ili waweze kulima kwa tija. (Makofi)

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzalisha Mbegu bora za Parachichi aina ya Hass na kuzigawa kwa wakulima kwa bei nafuu?

Supplementary Question 3

NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Naibu Waziri amekiri kwamba kuna uzalishaji holela wa miche hii ya maparachichi na katika mikoa inayolima parachichi, Songwe pia ni mkoa mmoja kati ya mikoa inayolima parachichi: Ni nini mkakati wa utoaji elimu kwa wananchi na wakulima ili waweze kuepukana na hawa matapeli, wazalishaji wa hizi mbegu? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kupitia mwongozo ambao tutautoa, utatoa mfumo mzima wa upatikanaji wa miche bora na yenye kuleta tija kwa wakulima wa parachichi na hivyo itaondoa changamoto iliyopo hivi sasa ambapo katika baadhi ya maeneo kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi, kuna chongomoto ya upatikana wa miche bora ya parachichi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kupitia mwongozo huu wa TOSCI, maana yake utakuwa ndiyo mwongozo utakaomfanya mkulima yeyote wa Tanzania ambaye anataka kulima parachichi ataufuata na itakuwa ni sehemu salama kwake kwa sababu ni taasisi ya Serikali ambayo itafanya kazi hii ya kuhakikisha kwamba wakulima wote wanapata miche bora.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzalisha Mbegu bora za Parachichi aina ya Hass na kuzigawa kwa wakulima kwa bei nafuu?

Supplementary Question 4

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa kumekuwa na changamoto kubwa sana ya upatikanaji wa mbegu za shayiri. Je, Serikali haioni sasa haja ya kuanzisha kituo cha uzalishaji wa mbegu katika shamba la NAFCO lililoko Wilaya ya Hanang?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba tu kumwambia Mheshimiwa Mbunge kwamba shamba la Bassotu kama Wizara, tunaligeuza kuwa ni center of excellence kwa ajili ya kuzalisha ngano na shairi.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzalisha Mbegu bora za Parachichi aina ya Hass na kuzigawa kwa wakulima kwa bei nafuu?

Supplementary Question 5

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, kigezo cha bei ya mche kinatokana na umri wa mche, kwa sababu hata sasa hivi kuna miche bora kabisa inapatikana kwa shilingi 3,000. Sasa swali langu; Serikali imetumia kigezo gani; ama itatumia kigezo gani cha umri, ili huo mche wa shilingi 2,000 usiwe tofauti na miche ya sasa ambayo inauzwa shilingi 3,000 kwa sababu umri wake ni mdogo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Halima Mdee, mkulima wa parachichi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema, zao hili la parachichi ni zao ambalo hivi sasa limeanza kukimbiliwa na wakulima wengi sana kwa sababu limeleta soko la uhakika na vilevile watu wameanza kunufaika kwa kiwango kikubwa sana.

Kuhusu suala la miche ambayo tutaizalisha, ni kweli liko suala la umri wa miche, lakini ni lazima tunanzie sehemu. Sehemu yenyewe ni kwamba, uzalishaji wetu wa miche kama nilivyosema, ni ule ambao tunaamini kabisa wakulima wa parachichi kupitia miche ambayo tutaizalisha chini ya vituo vyetu vya TARI, ambavyo itakuwa ni ya ndani ya muda mfupi pia, wapate kwa bei hiyo hiyo ambapo miche ile mingine ya muda mrefu imekuwa ikiuzwa.

Mheshimiwa Spika, lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba, ni lazima tuanzie sehemu, lakini mbele tutaboresha kuhakikisha ya kwamba, basi wakulima wetu wawe wana bei ambayo ni standard, ambayo kila mmoja anaweza akai- afford na mwisho wa siku tunaongeza tija katika kilimo chetu cha parachichi na hasa katika eneo ambalo Mheshimiwa Mbunge analima huko. (Makofi)

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzalisha Mbegu bora za Parachichi aina ya Hass na kuzigawa kwa wakulima kwa bei nafuu?

Supplementary Question 6

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa wananchi wa Jimbo la Hai, wamehamasika sana kulima zao hili la parachichi na zao la kahawa: Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa ruzuku ili wakulima hawa waweze kufanya kazi hii kwa ufanisi? Ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi, kutokana na umuhimu wa zao hilo la parachichi, Serikali tumedhamilia kuweka ruzuku ya kutosha ili kuwafanya wakulima waendelee kulima kwa tija na kupata miche hii kwa bei nafuu.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Mkoa wa Kilimanjaro, tunashirikiana pia na wadau kama Africado na wadau wengine kama vile KEDA kule Rombo ambao pia kwa pamoja tunafanya kazi ya uzalishaji wa parachichi. Tumesema katika bajeti ya mwaka 2022/2023, tutazungumza kuhusu ruzuku ambayo tumeitenga kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wakulima hawa wanapata miche kwa bei nafuu.