Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 10 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 85 2022-04-21

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuzalisha Mbegu bora za Parachichi aina ya Hass na kuzigawa kwa wakulima kwa bei nafuu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shally Josepha Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli miche ya parachichi katika baadhi ya maeneo imekuwa ikiuzwa kwa bei kati ya shilingi 5,000 hadi shilingi 6,000 ambapo baadhi ya wananchi wanashindwa kumudu, kwani ekari moja inahitaji miche siyo chini ya 70 na kwa ekari 10 utahitaji shilingi 3,500,000 kwa ajili ya miche tu iwapo bei ya mche ni shilingi 5,000.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali kupitia TARI inatarajia kuanza uzalishaji wa miche ya parachichi milioni 20. Miche hiyo itauzwa kwa bei ya ruzuku ya chini ya shilingi 2,000. Aidha, katika kudhibiti ubora wa wazalishaji binafsi, Serikali kupitia Taasisi ya Uthibiti Ubora wa Mbegu (TOSCI) imeanza usajili wa wazalishaji wa miche ya parachichi nchini. Pia katika kuhakikisha usimamizi bora wa zao hili, Serikali inatarajia kuzindua mwongozo wa uzalishaji wa zao la parachichi.