Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali italipa wananchi wa Kijiji cha Usulo, Kata ya Mbungani Tabora Manispaa, ambao maeneo yao yalichukuliwa na Jeshi?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, suala hili la Usule limekuwa ni la muda mrefu sana na hii mambo ya uhakiki na hawa akina mama watatu watalipwa fedha zao imekuwa ni muda mrefu sasa. Hebu Serikali itoe majibu ya uhakika, lini hasa hawa wamama watapata fedha zao. (Makofi)

Swali langu la pili, katika Kijiji hiki cha Usule kuna ranch ya Kalunde ambayo Wanajeshi pia walichukuwa maeneo hayo kwenye kaya 14 zaidi ya miaka kumi sasa watu hawa wanaambiwa wamefanyiwa uhakiki lakini hawajalipwa fedha zao. Serikali itoe kauli ya hawa wananchi 14 pia katika ranch ya Kalunde ni lini mtawapa fedha zao ili waende kwenye maeneo mengine waweze kufanya shughuli zao za maendeleo. (Makofi)

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, migogoro ya ardhi ina mchakato na kama unavyoona Mheshimiwa Mbunge mchakato umeshafika ukingoni, tumekwishafanya uhakiki vitabu vimeshaandaliwa na tayari imeshakubalika na fedha zimekwishatengwa. Kwa hiyo, naomba tu Mheshimiwa Mbunge na wananchi wavute subra kidogo ili waweze kulipwa, kwa sababu fedha tayari ziko katika bajeti ya mwaka huu wa fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili naomba nilijibu kwamba hii ni kero mpya, kwa hiyo tunaipokea na tutaifanyia kazi na kama itahitajika tutaingiza katika mpango wetu wa kutatua migogoro unaoendelea mpango wa miaka mitatu.

Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali italipa wananchi wa Kijiji cha Usulo, Kata ya Mbungani Tabora Manispaa, ambao maeneo yao yalichukuliwa na Jeshi?

Supplementary Question 2

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Madam Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la dogo nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hali iliyoko katika Kijiji cha Usule Mkoani Tabora inafanana kabisa na hali iliyoko Kjiji Tondoroni Wilaya ya Kisarawe, Kata ya Kiluvya Mkoani Pwani, sasa napenda kujua ni lini Serikali mtawalipa fidia wananchi wale au kurudisha yale maeneo ili waweze kuyaendeleza. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nitalijibu kwa ujumla nikianza kwa kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wengi ambao wamekwisha niona kufuatilia migogoro ya ardhi katika maeneo yao.

Mhesihimiwa Spika, niseme kwamba tunao mpango wa kusuluhisha hii migogoro baina ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania na wananchi ambao umejumuisha maeneo 152 yanayohusisha Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar. Mpaka sasa tumekwisha pima maeneo 86, tumekwisha fanya uthamini wa maeneo 13 na upimaji unaendelea katika maeneo 66, na mpango huu ni wa miaka Mitatu.

Mheshimiwa Spika, ninaomba baada ya kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote, maana wengi sana wamekwisha nifuata kwa ajili ya migogoro katika maeneo yao, nawashukuru na kuwapongeza ila niwaombe tu wavute subira tuweze kukamilisha hii michakato inayoendelea. Ahsante.