Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 9 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 80 2022-04-20

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italipa wananchi wa Kijiji cha Usulo, Kata ya Mbungani Tabora Manispaa, ambao maeneo yao yalichukuliwa na Jeshi?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa inakiri kuwa walikuwepo wananchi watatu katika eneo hilo kabla halijachukuliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania. Manispaa ya Tabora imekishafanya uthamini na vitabu vya uthamini viliwasilishwa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Septemba mwaka 2021, Wizara imekwishawasilisha vitabu hivyo Wizara ya Fedha na Mipango kwa ajili ya uhakiki na uhakiki ulikamilika Disemba mwaka 2021.

Mheshimiwa Spika, fedha kwa ajili ya fidia zimejumuishwa katika bajeti ya Wizara ya Mwaka wa Fedha huu unaoendelea 2021/2022 na inatarajiwa kuwa wananchi husika watalipwa fedha hivi karibuni, mara baada ya Wizara kupokea fedha hizo kutoka Wizara ya Fedha na Mipango.