Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. FLORENCE G. SAMIZI K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa Watumishi wa Kada mbalimbali katika Hospitali nchini pamoja na ukosefu wa Vifaa tiba?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Tunaendelea kuishukuru Serikali kwa jinsi ambavyo inaendelea kupambana kuongeza vituo vya afya na vifaa kama ilivyojielekeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo changamoto kubwa ya watumishi kutokukaa katika vituo vya afya ni ukosefu wa nyumba.

Je, nini mkakati wa Serikali kuwajengea watumishi wa afya nyumba ili waweze kukaa kwenye vituo hivyo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dokta Florence Mbunge wa Muhambwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tuna upungufu wa nyumba za watumishi katika vituo vyetu na mpango wa Serikali sasa ni kuendelea kutenga fedha kupitia mapato ya ndani lakini pia kutoka Serikali Kuu kuhakikisha nyumba za watumishi zinajengwa. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mpango huu tayari umeratibiwa.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. FLORENCE G. SAMIZI K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa Watumishi wa Kada mbalimbali katika Hospitali nchini pamoja na ukosefu wa Vifaa tiba?

Supplementary Question 2

MHE. JUSTINE L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, ninataka kujua ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba na watumishi katika zahanati za Lugalo, Masege na Mbawi pia katika vituo vya afya vya Ruaha Mbuyuni, Ilula na Mluhe.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Justin Nyamoga Mbunge wa Jimbo la Kilolo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vituo vyote ambavyo amevitaja ni kipaumbele cha Serikali kuhakikisha vinapelekewa vifaa tiba na watumishi na ndiyo maana tunakwenda kuajiri watumishi 7,600 mwaka huu wa fedha pia tumetenga Shilingi Bilioni 69.95 kwa ajili ya vifaa tiba. Nimhakikishie kwamba tutatoa kipaumbele katika vituo hivyo. Ahsante.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLORENCE G. SAMIZI K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa Watumishi wa Kada mbalimbali katika Hospitali nchini pamoja na ukosefu wa Vifaa tiba?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa, kuna upungufu mkubwa wa watumishi katika hospitali zetu Wilaya ya Itilima na Wilaya ya Busega. Je, ni lini Serikali italeta watumishi wa kutosha katika Wilaya hizo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Itilima na Busega ni moja ya Halmashauri zenye upungufu wa watumishi lakini zitapewa kipaumbele kwenye ajira hizi ambazo zimekwishatangazwa. Ahsante.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. FLORENCE G. SAMIZI K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa Watumishi wa Kada mbalimbali katika Hospitali nchini pamoja na ukosefu wa Vifaa tiba?

Supplementary Question 4

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana Wilaya ya Kishapu ina vituo vya afya vitatu ambavyo vimekamilika na vimeanza kufanyakazi lakini kuna tatizo kubwa la upungufu wa watumishi katika vituo hivyo vya Dulisi, Mwangalanga pamoja na Mwigumbi.

Je, ni lini Serikali italeta watumishi wa kutosha pamoja na tatizo zima la vifaa tiba kushughulikiwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Butondo Mbunge wa Jimbo la Kishapu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli vituo ambavyo amevitaja vina upungufu wa vifaa tiba lakini pia upungufu wa watumishi. Kama ambavyo nimejibu kwenye maswali mengine ya nyongeza na swali la msingi kwamba Serikali imeweka kipaumbele cha kuajiri watumishi na kuwapeleka kwenye vituo hivyo lakini pia kuhakikisha tunanunua vifaa tiba na kupeleka kwenye vituo hivyo. Nimhakikishie Mheshimiwa Butondo kwamba Jimbo lake la Kishapu nalo litapewa kipaumbele. Ahsante.

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLORENCE G. SAMIZI K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa Watumishi wa Kada mbalimbali katika Hospitali nchini pamoja na ukosefu wa Vifaa tiba?

Supplementary Question 5

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe ikiwepo ultrasound pamoja na x-ray? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martha Mariki Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ukosefu wa vifaa tiba katika Hospitali ya Halmashauri ya Mpimbwe lakini hospitali zingine za Halmashauri na vituo vya afya ni kipaumbele cha Serikali nimuhakikishe Mheshimiwa Mbunge katika bajeti hii inayokuja lakini watumishi ambao wanaajiriwa katika mwaka huu wa fedha tutakipa kipaumbele kituo hiki cha afya na Hospitali ya Halmashauri ya Mpimbwe. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLORENCE G. SAMIZI K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa Watumishi wa Kada mbalimbali katika Hospitali nchini pamoja na ukosefu wa Vifaa tiba?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Na mimi naomba kuuliza katika Mkoa wetu wa Pwani katika Wilaya ya Kibiti tuna hospitali ya Mbochi na Mwambao ambayo imekamilika. Ni lini Serikali mtaleta vifaa tiba? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Alice Kaijage Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwenye vifaa ambavyo vitakwenda kununuliwa kwenye mwaka wa fedha ujao tutatoa kipaumbele katika hospitali hii ambayo inahitaji vifaa tiba. Ahsante.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLORENCE G. SAMIZI K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa Watumishi wa Kada mbalimbali katika Hospitali nchini pamoja na ukosefu wa Vifaa tiba?

Supplementary Question 7

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Hospitali ya Wilaya ya Kyerwa haina watumishi na hivyo kupelekea wagonjwa wengi kujazana kwenye kituo cha afya cha Nkwenda. Sasa nataka kujua ni lini na ni kwa kipaumbele kiwango gani hiyo hospitali itapewa ili kupunguza adha ambayo kituo cha afya cha Nkwenda inapitia kuwa na wagonjwa wengi.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Theonest Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya Kyerwa ina upungufu wa watumishi pamoja na vituo vingine vya afya, lakini nimpongeze Mheshimiwa Mbunge ambavyo ameendelea kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kyerwa ambaye mara kwa mara amekuwa anakumbushia kuhusiana na watumishi katika eneo hilo nimhakikishie kwamba tutaipa kipaumbele cha watumishi hospitali ya Wilaya ya Kyerwa. Ahsante sana. (Makofi)