Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 75 2022-04-20

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLORENCE G. SAMIZI K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa Watumishi wa Kada mbalimbali katika Hospitali nchini pamoja na ukosefu wa Vifaa tiba?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2020/2021 iliajiri Watumishi wa kada za afya 2,726 ambao walipelekwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali inatarajia kuajiri watumishi 7,612 wa kada mbalimbali za afya ambao watapelekwa kwenye Halmashauri zote nchini.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais - TAMISEMI imetenga Shilingi Bilioni 69.95 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba kwa Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali za Halmashauri zilizokamilika.