Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaziba nakisi ya uagizaji mafuta ya kula kwa kuruhusu uwekezaji mkubwa katika Bonde la Ziwa Tanganyika?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika ahsante, kwa kuwa zao la chikichi linastawi vizuri katika Bonde la Tanganyika na kwa kuwa chikichi inazalisha mafuta, lakini pia malighafi kwa ajili ya kutengenezea sabuni lakini pia mabaki yake yanatumika katika uzalishaji wa chakula cha mifugo.

Je, ni mkakati upi Serikali inauweka kutafuta wawekezaji wakubwa kama wale wa mashamba ya miwa katika bonde hili ili angalau kuziba nakisi hii? Ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali ni kuanza kuzungumza na wawekezaji wakubwa walionesha nia kuwekeza katika eneo ikiwemo Kampuni ya Wilmar, Kampuni ya Bakhresa na Mohamed Enterprises na mazungumzo yanakwenda vizuri na wako tayari kufanya uwekezaji huo pindi pale mashamba makubwa yatakapopatikana na tayari mashamba hayo hivi sasa wataalamu wetu wa Wizara ya Kilimo wapo kule kwa ajili ya upimaji wa afya ya udongo ili tukijiridhisha basi tuweze kukaa chini kuzungumza na hawa wawekezaji watumie mashamba hayo makubwa kwa ajili ya uzalishaji wa chikichi.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaziba nakisi ya uagizaji mafuta ya kula kwa kuruhusu uwekezaji mkubwa katika Bonde la Ziwa Tanganyika?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Spika, ahsante; nini mkakati wa Serikali wa kuzalisha zao la karanga ili kuweza kuchakata mafuta ya karanga na kupunguza uagizaji mafuta kutoka nje? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Fatma Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkakati mkubwa tulionao hivi sasa ni kuendelea kuisisitiza taasisi yetu ya kilimo (TARI) katika kuendelea kufanya utafiti na uzalishaji wa mbegu bora ili wakulima waweze kulima kwa tija na mwisho wa siku kama nchi tuweze kufikia malengo ya kuondokana na changamoto ya uagizaji wa mafuta.

Kwa hiyo, mazao ambayo tumeyapa kipaumbele katika kukamua mafuta ni pamoja na karanga, mchikichi pamoja na alizeti. Kwa hiyo, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge nisehemu ya mkakati wa Wizara.