Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Haji Makame Mlenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza: - Je, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi inashirikiana vipi na Ofisi ya Makamu wa Rais kuweka mazingira mazuri kandokando ya barabara?

Supplementary Question 1

MHE. HAJI MAKAME MLENGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuweza kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini pia naomba kuuliza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa baadhi ya viwanda au baadhi ya wadau mbalimbali hutengeneza bustani nzuri tu kandokando ya barabara, lakini hulipishwa fedha nyingi na Wizara yako.

Je, huoni sasa ni muda muafaka wa kuondoa tozo hizo ili wadau hao waendelee kutengeneza bustani nzuri hasa katika maeneo ya majiji yetu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Wizara yako ina mkakati gani wa kuwatia moyo wale wote wanaotengeneza bustani nzuri kando kando ya majiji badala ya kuwalipisha fedha nyingi pale wanapofanya hivyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Haji Makame Mlenge, Mbunge wa Chwaka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tuna kitu kinachoitwa road maintenance manual ambacho ni kama mwongozo wa watu wote ambao wanaomba kutumia hifadhi ya barabara na kule ndiyo tumetaja gharama ya kila shughuli ambayo mtu anaifanya ikiwepo ni pamoja na kuweka bustani kando kando ya barabara.

Kwa hiyo, tuna mwongozo ambao upo, lakini kama bei ni kubwa, tutalichukua na kuliangalia kama limekuwa ni changamoto kwa watu ambao wanatumia eneo la kandokando ya barabara kwa ajili ya kutunza mazingira na kupendezesha mji.

Mheshimiwa Spika, kwenye suala la pili kama alivyosema, sisi tuko tayari kukaa na hao watu ili tuwatie moyo na bado nafasi huwa zinatangazwa, yaani kwamba barabara ikishajengwa unaruhusiwa kwenda kuomba na kupewa kibali cha kuweka shughuli ambazo siyo za kudumu kandokando ya barabara ikiwa ni kutunza mazingira na kupendezesha miji, na kwa miji tunashirikiana sisi na wenzetu wa TAMISEMI ambao wana barabara nyingi katika miji, majiji na manispaa, ahsante.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza: - Je, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi inashirikiana vipi na Ofisi ya Makamu wa Rais kuweka mazingira mazuri kandokando ya barabara?

Supplementary Question 2

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi.

Mheshimiwa Spika, uchafuzi wa mazingira kwenye nchi yetu ni jambo ambalo linaendelea kushamiri sana, kwa mfano unaweza wakati unatoka Dar es Salaam labda kuelekea Momba, ukapita sehemu kabisa hakuna makazi ya watu, lakini utakuta takataka nyingi sana zimejaa barabarani.

Je, Serikali haioni kuchukua ushauri huu kutumia vijana wetu ambao wako mtaani hawajapata ajira waliomaliza ngazi za certificate, diploma na hususan wale ambao wamepitia na jeshini hawajapata ajira. Je, hamuoni muanzishe programu maalum kwa ajili vijana hawa kutunza mazingira yetu ikiwa ni pamoja na kuweka faini kwa mtu yeyote ambaye atabainika anatupa takataka hovyo ili kipato pia cha kuwalipa vijana hawa kitokane na faini ambazo tutakuwa tunatozwa sisi wenyewe Watanzania kwa kutokutunza mazingira yetu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Condester Sichalwe, Mbunge wa Momba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza siyo utaratibu kwa mtu unaposafiri na kutupa takataka nje. Naomba suala hili niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge na Watanzania kwa ujumla kwamba siyo outaratibu na ndiyo maana magari mengi ya usafiri sasa hivi kuna utaratibu ambao kunakuwa na dustbin ambayo mtu yeyote msafiri anatakiwa aweke uchafu na mahali tukifika gari basi watakwenda kutupa takataka.

Mheshimiwa Spika, ushauri wa vijana nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tumeuchukua kusaidiana na wenzetu wanaotunza miji ambao ni TAMISEMI kuona namna wanavyoweza kufanya kunapotokea uchafu mbalimbali kando kando ya barabara zetu.