Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 142 2023-02-10

Name

Haji Makame Mlenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza: -

Je, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi inashirikiana vipi na Ofisi ya Makamu wa Rais kuweka mazingira mazuri kandokando ya barabara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Haji Makame Mlenge, Mbunge wa Chwaka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kuweka mazingira mazuri kandokando ya barabara, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi inashirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kuhamasisha utunzaji wa mazingira ya barabara ikiwa ni pamoja na upandaji miti kandokando ya barabara. Aidha, Wizara inaendelea kuzingatia Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021, Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na Miongozo ya Usimamizi wa Mazingira katika kutunza mazingira ya barabara.

Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais kupitia NEMC inaendelea kuzingatia sheria hiyo kwa kuhakikisha miradi ya barabara inafanyiwa Tathmini ya Athari kwa Mazingira (Environmental Impact Assessment) kabla ya ujenzi na kufanyia kazi matokeo ya tathmini hiyo ili kutunza mazingira ikiwemo kuweka mazingira mazuri kandokando ya barabara, ahsante.