Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, kwa mujibu wa tafiti ni madini aina gani yanapatikana katika Mkoa wa Rukwa na katika maeneo gani?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, na ninaomba niishukuru Serikali kwa majibu yake mazuri ambayo yamesheheni taarifa za kutosha. Naomba niulize maswali madogo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba pamoja na hayo madini ambayo yametajwa kwa idadi kubwa shughuli ya uchumi kwa maana ya uchimbaji haijaanza kufanyika, na hii inawezekana ni kwa sababu hamasa na elimu haijatolewa kwa ajili ya wananchi kuweza kuchimba.

Je, Serikali iko tayari kutoa hamasa na elimu ili wananchi waanze kuchimba madini hayo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika taarifa ambayo imetajwa na Serikali imetajwa kwa ujumla kwa mfano Kata ya Katazi.

Je, Serikali iko tayari kufanya utafiti wa kina kujua exactly deposit hiyo inapatikana wapi? ahsante.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa swali lake la kwanza; ni kweli uchimbaji bado haujapata kasi katika wilaya yake, lakini nimhakikishie kwamba, kama ni kutokana na uelewa mdogo Tume ya Madini wamejipanga kuzunguka nchi nzima kuhamasisha wachimbaji wadogo katika maeneo yenye madini ili waweze kujipanga waunde vikundi na tuweze kuwasaidia kwa ukaribu wafaidike na madini waliyonayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa swali lake la pili ni kweli taarifa hizi tulizozitoa hapa ni taarifa za utafiti wa awali unaofanywa na taasisi yetu ya GST, lakini utafiti wa kina ufanywe kwa kutumia vifaa vya kisasa vya uchongaji. Na kutambua umuhimu wa kuwasaidia wachimbaji wadogo Wizara ya Madini imeagiza kupitia Taasisi yake ya STAMICO mitambo mitano ya kuwasaidia wachimbaji wadogo wafahamu kiwango cha madini kinachopatikana katika maeneo yao ili wanapokwenda kuanza kuzalisha wachimbe madini wakiwa na uhakika kwamba watapata tija kutokana na juhudi zao. Ahsante sana.