Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Madini 120 2023-02-08

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: -

Je, kwa mujibu wa tafiti ni madini aina gani yanapatikana katika Mkoa wa Rukwa na katika maeneo gani?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege Mbunge wa Jimbo la Kalambo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Rukwa ni miongoni mwa mikoa iliyobarikiwa kuwa na madini ya aina mbalimbali. Kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) mkoa huu una madini yafuatayo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Dhahabu katika kata za Kabwe, Namanyere, Msenga na Ninde. Shaba katika Kata za Kirando, Namanyere, Msenga, Kala na Ninde. Risasi katika Kata za Namanyere na Ninde, Makaa ya Mawe katika Kata za Chala, Kipande, Muze na Ntendo. Madini ya viwandani kuna chokaa Kata ya Ntendo, na Kyanite Kata ya Msenga. Chumvi Kata za Kirando, na Kipeta. Ulanga Kata za Mkwamba, Mwazye, Kaoze na Senga. Vito katika Kata za Chala, Kipande, Senga na Malangali. Rare Earth Elements Kata za Mkwamba na Msenga. Chemichemi za majimoto zenye kuambatana na gesi ya helium katika Kata za Kirando na Msenga, na Chuma katika Kata ya Katazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, madini mengine ni madini ujenzi ambayo ni kokoto na mchanga ambayo yanapatikana katika Wilaya zote za Mkoa wa Rukwa ahsante sana.