Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutatua changamoto ya uhaba wa walimu katika shule za pembezoni?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, pamoja na majibu mazuri ya Serikali lakini bado kumekuwa kuna changamoto kubwa hususan kwa shule shikizi ambazo zilipata msaada kupitia maswala la UVIKO pamoja na kupitia Kapu la Mama.

Je, Serikali inatoa tamko gani kuhusiana na shule hizo kupatiwa walimu ikiwa shile hizo zimesajiliwa lakini nyingi zina mwalimu mmoja mmoja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili, pamoja na kuonekana kwamba kada ya walimu imekuwa ikiajiri sana walimu wakike lakini kwa Mkoa wa Katavi imekuwa ni tofauti. Katika Mkoa wetu wa Katavi kuna changamoto kubwa sana ya walimu wa kike katika shule za Sekondari; mfano katika shule ya Majalila, shule ya Mwamapuli ambapo shule hizo zimekuwa hazina kabisa walimu wa kike.

Je, Serikali inatoa tamko gani ili Watoto wetu waweze kupata mahitaji ambayo mtoto wa kike anayapata akiwa na mwalimu wa kike shuleni?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Martha Festo Mariki, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua uwepo wa vituo shikizi ambavyo vinasaidia shule mama. Tulishatoa maelekezo kwa Makatibu Tawala wote mikoa nchini kuhakikisha kwamba wanafanya msawazo na sehemu ya msawazo huo ni pamoja na kupeleka walimu kwenye hivo vituo. Kwa hiyo nirudie tena jmabo hili litekelezwe kama ambavyo Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais- TAMISEMI amekwishalitolea maelekezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kuhusu walimu wa kike Mkoa wa Katavi kukosekana, tumelipokea ili tulifanyie kazi kwa kuongeza idadi ya waalimu katika ajira zinazofuatia, na katika maeneo ambayo kuna walimu wengi tutafanya msawazo vilevile kuwapeleka katika maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameainisha, ahsante sana.