Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itazijenga barabara za Kibada – Mwasonga – Tundwi – Songani na Ngomvi – Kimbiji hadi Pembamnazi kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Wizara ya Ujenzi na majibu yenye faraja kwa wakazi wa Kigamboni hususan maeneo ya Mwasonga, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Wizara ya Ujenzi kupitia TANROADS ilifanya ujenzi wa kipande kidogo cha kilometa moja kutoka Kibada junction kwenda Mwasonga. Sasa hivi ni zaidi ya mwaka mmoja na nusu, kipande kile cha kilometa moja hakijakamilika.

Je, ni lini sasa Serikali itakamilisha ujenzi wa kile kipande cha kilometa moja ambao ujenzi wake umeanza? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; barabara nyingi pale Kigamboni zimemeguka kutokana na kukosa kingo kutokana na magari mazito kuchepuka nje ya barabara na kwingine barabara zimekatwa kashata kutokana na ubovu lakini hazijakarabatiwa. Sasa ni lini barabara zile zitakarabatiwa lakini vile vile kuwekwa kingo ili barabara zile zisiendelee kumomonyoka? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Faustine Engelbert Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli mkandarasi ambaye alipewa kazi ya kukamilisha kipande cha kilometa moja amechelewa na tayari ameshaandikiwa barua na anatumikia adhabu ya liquidated damage na kama atakuwa hajakamilisha ndani ya siku 100, tunafunga mkataba kumtafuta mkandarasi mwingine. Hivi tunavyoongea yupo anakamilisha hiyo kazi na yuko kwenye 75%-80%.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mashimo na kingo za barabara, tayari tumesham-engage mkandarasi, Mark Construction na ameshaanza kazi na kuharibika kwa barabara hii ni kweli ni barabara ya zamani, traffic imeongezeka sana na magari mengi makubwa yanapita. Kwa hiyo tayari mkandarasi yupo kwa ajili ya kukarabati barabara hizo za lami. Pia hata hizo za changarawe tumeshamweka mkandarasi kuhakikisha kwamba anakarabati hizo barabara, ahsante. (Makofi)

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itazijenga barabara za Kibada – Mwasonga – Tundwi – Songani na Ngomvi – Kimbiji hadi Pembamnazi kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ni lini Barabara ya Masasi – Nachingwea - Liwale itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tecla Ungele, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja sasa hivi zinafanyiwa evaluation, ndiyo moja ya barabara ambazo ziko kwenye EPC+F. Ahsante. (Makofi)

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itazijenga barabara za Kibada – Mwasonga – Tundwi – Songani na Ngomvi – Kimbiji hadi Pembamnazi kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Kwa kuwa Barabara ya Mbalizi - Shigamba ni ahadi ya muda mrefu ya viongozi wetu na pia ni kiungo muhimu kwa Tanzania na Malawi. Je, ni lini itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oran Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tunavyoongea sasa hivi, Mhandisi Mshauri yuko site akifanya usanifu wa kina na baada ya hapo, barabara hii itatafutiwa fedha kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itazijenga barabara za Kibada – Mwasonga – Tundwi – Songani na Ngomvi – Kimbiji hadi Pembamnazi kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kumekuwa na ahadi ya muda mrefu ya kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Karatu – Njiapanda - Mang’ola - Lalago kwa kiwango cha lami. Je, ni lini ahadi hii itatekelezwa ili barabara hiyo ijengwe kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ahadi hiyo ipo ya kujenga hiyo barabara ya Karatu hadi Lalago kwa kiwango cha lami. Serikali bado haijaufuta mpango huo, inaendelea kutafuta fedha na fedha zikipatikana basi barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itazijenga barabara za Kibada – Mwasonga – Tundwi – Songani na Ngomvi – Kimbiji hadi Pembamnazi kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nataka kujua ni lini Barabara ya Nyakanga kwenda Nyaishozi kuja mpaka Benako itajengwa kwa kiwango cha lami, kwa sababu ni barabara kuu inaunganisha Tanzania na Rwanda?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii tumeshaanza kuijenga kwa kiwango cha lami kilometa 60 na barabara iliyobaki, African Development Bank wako kwenye majadiliano ili kuikamilisha yote kuunganisha Tanzania, Burundi na Rwanda.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itazijenga barabara za Kibada – Mwasonga – Tundwi – Songani na Ngomvi – Kimbiji hadi Pembamnazi kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Barabara ya Dar es Salaam inaunganisha baina ya Dar es Salaam na Pwani. Vilevile barabara hizi ni kiunganishi kati ya Mkuranga na Ilala ambayo ni Kiguza – Hoyoyo – Mwanadilatu - Msongola. Sasa lini barabara hizi zitajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salma Kikwete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hizi ni muhimu kama alivyozitaja na zinaunganisha barabara kuu na barabara hizi ambazo tunasema ni feeder roads. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kufanya usanifu wa kina na baadaye ziweze kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itazijenga barabara za Kibada – Mwasonga – Tundwi – Songani na Ngomvi – Kimbiji hadi Pembamnazi kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya swali la nyongeza. Barabara ya kutoka Kiranjeranje - Makangaga – Nakiu - Nanjilinji na hatimaye Ruangwa imefikia hatua gani ili ijengwe kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii imeshafanyiwa usanifu na Serikali inatafuta fedha kuijenga hii barabara kwa kiwango cha lami kuanzia Kiranjeranje hadi Ruangwa, ahsante.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itazijenga barabara za Kibada – Mwasonga – Tundwi – Songani na Ngomvi – Kimbiji hadi Pembamnazi kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Je, ni lini Serikali itajenga Barabara ya Mogitu - Hydom kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, barabara aliyotaja Mheshimiwa Hhayuma, ni link kati ya Barabara ya Babati - Hydom kwenda Sibiti. Kwa hiyo itakavyoanza kujengwa, hicho kipande kitakuwa ni sehemu ya hiyo barabara.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itazijenga barabara za Kibada – Mwasonga – Tundwi – Songani na Ngomvi – Kimbiji hadi Pembamnazi kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 9

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kuuliza swali, barabara ya kutoka Chimara kwa maana ya Mfumbi kuelekea Matamba-Kitulo, kilometa 51. Barabara ambayo inaelekea kwenye hifadhi ya utalii. Ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hii kwa sababu upembuzi yakinifu ulishaanza kufanyika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sanga, Mbunge wa Makete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuifungua barabara hii kwa ajili ya kuunganisha maeneo ya Chimara - Itamba hadi Makete, lakini pia tunajua tutakuwa tunafungua utalii eneo hilo, ahsante.

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itazijenga barabara za Kibada – Mwasonga – Tundwi – Songani na Ngomvi – Kimbiji hadi Pembamnazi kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 10

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa barabara ya kutoka Mtwara mpaka Msimbati, ambayo takribani sasa ina zaidi ya miaka 15, barabara hii inajengwa kwa vipande vipande? Sasa hivi wamejenga kilometa tano tu. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtenga, Mbunge wa Mtwara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii tunajenga kwa awamu kadiri fedha inavyopatikana. Azma ya Serikali ni kujenga barabara yote. Kwa hiyo Serikali inatafuta fedha ili zikikamilika basi tuweze kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itazijenga barabara za Kibada – Mwasonga – Tundwi – Songani na Ngomvi – Kimbiji hadi Pembamnazi kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 11

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kufanya upembuzi yakinifu Barabara ya kutoka Nyoni hadi Mipotopoto-Mitomoni kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Engineer Manyanya, Mbunge wa Nyasa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ipo kwenye ilani hii barabara kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami na tunategemea katika bajeti ijayo iweze kuingia ili iweze kufanyiwa usanifu wa kina ikiwa ni maandalizi ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.