Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 6 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 103 2023-02-07

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itazijenga barabara za Kibada – Mwasonga – Tundwi – Songani na Ngomvi – Kimbiji hadi Pembamnazi kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa naiaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninapenda kujibu Swali la Mheshimiwa Faustine Engelbert Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, zabuni kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami kwa Barabara ya Kibada-Mwasonga, Tundwi-Songani hadi Kimbiji yenye urefu wa kilometa 41 zimetangazwa tarehe 6 Januari, 2023 na zitafunguliwa tarehe 17 Februari, 2023. Kwa upande wa Barabara ya Ngomvu – Kimbiji hadi Pemba Mnazi yenye urefu wa kilometa 27, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umekamilika na sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha za kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami, ahsante.