Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga majosho ya kuogesha mifugo katika Halmashauri ya Msalala?

Supplementary Question 1

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwanza niipongeze Serikali kwa kutenga fedha kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kwa ajili ya ukarabati wa majosho matano. Nilitaka kuuliza swali langu la kwanza, kama Serikali ilitenga fedha kukarabati majosho haya Matano;

Je, fedha zilizotengwa kwenda kukarabati majosho Kata ya Ngaya na Ntobo zilikwendwa wapi na kama zipo Wizarani, ni lini sasa fedha hizo zitakuja kukarabati majosho hayo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa tulipokea barua iliyotuonesha kwamba tutaletewa majosho Matano, na Mkeka uliotoka, kwa maana ya idadi ya majosho ya mwaka huu haijaonyesha Msalala kuwemo.

Je, ni lini sasa Wizara itatuletea majosho hayo? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza; majosho mawili pesa zake hazifahamiki zilipo na kwa hivyo ninaomba nimueleze tu kwa mujibu wa utaratibu wa ujenzi wa majosho haya. Utaratibu wote wa manunuzi hufanywa na halmashauri ya wilaya. Baada ya kuwa wamekamilisha taratibu zote za manunuzi hutuletea Wizarani ambapo Katibu Mkuu wa Mifugo huenda kuziombea pesa zile Hazina. Ikiwa kama katika kata alizozitaja na hivyo vijiji alivyovitaja liko hilo tatizo, niko tayari mimi kumpa ushirikiano Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, kufanya uchunguzi kwa kutumia wataalam wetu ili tuweze kubaini wapi mkwamo huu ulikotokea na baadaye kuweza kuwanusuru wananchi wa pale Msalala.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ni hili la kata alizozitaja ambazo zilikuwepo lakini sasa anaona katika mkeka huu wa mwaka huu hazipo. Naomba nimuhakikishie, Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imetenga pesa za kutosha na mpaka sasa tumeshapeleka kiasi cha shilingi bilioni 5.4. Naomba nimuhakikishie tena kwa mara nyingine Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi hivi vijiji vinavyohitaji na anavyosema vilikuwepo katika mkeka nivipate tena ili tuweze kufanya ufuatiliaji wa pamoja wa kuona wapi palikosewa tuparekebishe na hatimaye wananchi wale waweze kupata ile huduma ya josho na hatimaye kuhudumia mifugo ile. Ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga majosho ya kuogesha mifugo katika Halmashauri ya Msalala?

Supplementary Question 2

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwenye Tarafa yangu ya Ingo yenye kata kumi na Ichuku kata tano, Inano kata tano hakuna josho hata moja katika eneo hilo. Nini mpango wa Serikali?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, namuomba Mheshimiwa Waitara aainishe mahitaji yake, ashirikiane na Mkurugenzi wake Mtendaji alete Wizarani tutamhudumia kwa jambo hili katika Bajeti ya Mwaka 2023/2024 ambayo tunaielekea sasa. Ahsante.

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga majosho ya kuogesha mifugo katika Halmashauri ya Msalala?

Supplementary Question 3

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Wakati Mheshimiwa Naibu Waziri alipofanya ziara kule Wilayani Simanjiro aliahidi Serikali kuipatia Wilaya ya Simanjiro majosho 22 lakini mpaka sasa tumepokea majosho mawaili tu. Je, Serikali ni lini itajenga majosho katika vijiji vyote ambavyo havina kabisa?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Regina, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Manyara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, maombi yalikuwa ni vijiji 22, hadi sasa wamepata majosho mawili. Mgawanyo wa majosho haya nchi nzima ni mkubwa kwa mahitaji na kwa hivyo huwa tunatenga kulingana na bajeti yetu. Haya waliyoyapata ni mwanzo na zoezi la kuendelea kupangiwa fedha linaendelea, tayari nimeshazungumza na Mheshimiwa Ole-Sendeka, alinisisitiza kuhakikisha kwamba yale yaliyosalia tuyapate. Ninataka nikuhakikishie Mheshimiwa Regina na Mheshimiwa Ole-Sendeka na Wanasimanjiro, mtapata; katika bajeti zinazoendelea kutengwa na ninyi Simanjiro mtaendelea kupata fedha hizo.