Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: - Je, ni lini chujio la maji linalojengwa katika Manispaa ya Mtwara Mikindani litakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu hayo, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kama chujio limekamilika kujengwa, kwanini maji yanatoka machafu na wakati mwingine wananchi wanashindwa kuyatumia?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; Mkataba wa uboreshaji wa miiundombinu ya maji katika Manispaa ya Mtwara Mikindani wenye thamani ya Shilingi bilioni 19 ulisainiwa mbele ya Mheshimiwa Waziri. Nataka kujua utekelezaji wake umefikia hatua gani? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tunza Malapo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la maji kutoka machafu baada ya ukamilishaji wa chujio ni suala la kiufundi. Ni sehemu chache ambapo mabomba ni chakavu wakati fulani bado yanaleta udongo kwa ndani lakini tayari watendaji wetu wanalifanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la mkataba kusainiwa mbele ya Mheshimiwa Waziri uko sahihi, tayari Shilingi bilioni 19 zimetengwa, Mkandarasi ameshapatikana, yuko kwenye mobilization, anafanya uandaaji wa site na hivi punde atalipwa advance payment ili kazi zianze.