Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 91 2023-02-07

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: -

Je, ni lini chujio la maji linalojengwa katika Manispaa ya Mtwara Mikindani litakamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekamilika ujenzi wa chujio la kuchujia maji mwezi Aprili, 2022. Kukamilika kwa ujenzi wa chujio hilo kumeweza kuboresha upatikanaji wa huduma ya majisafi na salama kwa wananchi katika Manispaa ya Mtwara Mikindani.