Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Maabara kwenye Zahanati zote za Jimbo la Kalenga?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri ninalo swali la nyongeza.

Kwa kuwa mgonjwa anapofika hospitalini hawezi kupata matibabu sahihi bila kupata vipimo; je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuhakikisha zahanati zote nchini zinapata maabara ili kutoa huduma sahihi kwa wagonjwa wetu? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mariam Kisangi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba ili upate huduma bora za afya lazima vipimo vya maabara vifanyike na Serikali kwanza imechukua hatua ya kuboresha ramani za majengo ya zahanati kwa kuongeza vyumba kutoka sita hadi vyumba 15, ambavyo vitawezesha kuwa na jengo zuri ambalo linakidhi huduma za maabara katika zahanati zetu.

Mheshimiwa Naibu Sspika, pili, zahanati zetu ambazo zilijengwa miaka ya nyuma ambazo hazikuwa na nafasi nzuri kwa ajili ya huduma za maabara, tumetenga maeneo ambayo huduma za maabara za msingi, kwa mfano vipimo vya malaria, vipimo vya wingi wa damu vinafanyika katika vyumba ambavyo vimekuwa improvised na huduma hizi zinaendelea kutolewa katika maeneo haya. Ahsante.