Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 87 2023-02-07

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Maabara kwenye Zahanati zote za Jimbo la Kalenga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Kalenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya afya kwa kujenga na kukarabati vituo vya kutolea huduma za afya katika ngazi ya afya ya msingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali ilipeleka fedha shilingi bilioni 27.8 kukamilisha maboma ya zahanati 555. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga shilingi bilioni 15 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa maboma ya zahanati 300.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Kalenga lina jumla ya zahanati 36 na kati ya hizo, zahanati 11 zinatoa huduma za maabara na zahanati 25 zinatoa huduma za maabara za msingi. Ili kuboresha huduma, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya kutolea huduma za maabara katika zahanati zote nchini zikiwepo zahanati za Jimbo la Kalenga, ahsante.