Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini minara ya mawasiliano itapelekwa Kata za Nyamtukuza, Nyabibuye, Gwarama, Kasuga, Rugenge, Gwanumpu, Katanga na Magunzu?

Supplementary Question 1

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Kakonko au Jimbo la Buyungu lina Kata 13. Kata zenye uhakika wa mawasiliano ni tano tu. Kutokana na hali hii, ndiyo imepelekea kuleta swali hapa Bungeni.

Je, Serikali inatoa kauli gani kwa kata nane ambazo ni Nyamutukuza, Nyabibuye, Gwarama, Kasoga, Rugenge, Gwanombo, Katanga na Mgunzu ambazo bado zina matatizo ya mawasiliano ya simu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kufuatana nami Buyungu ili aweze kuliona na kubaini tatizo hili ambalo nalitaja sasa? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Buyungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Aloyce kwa kazi kubwa anayoifanya, na kwa kweli ameendelea kushirikiana na Wizara kuhakikisha kwamba tunatatua changamoto za mawasiliano ndani ya jimbo lake.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa katika Jimbo ambalo lina Kata 13, Kata tano zina uhakika lakini vile vile kuna Kata karibia tano nyingine ambazo mawasiliano yapo lakini bado kuna changamoto mbalimbali ambazo naamini baada ya kuzifanyia kazi tatizo lake litaisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nitumie fursa hii, kwa sababu kwa uwepo wa TCRA kwa mujibu wa Sheria Na. 12 ya mwaka 2003, inaipa TCRA mamlaka ya kuhakikisha huduma ya mawasiliano inatolewa kwa ubora unaotakiwa. Sasa niwatake waende katika Jimbo la Buyungu wahakikishe kwamba wanaenda kufuatilia na kuangalia quality of service kama inaridhisha katika jimbo hili ili wananchi wa Buyungu waweze kupata huduma ya mawasiliano ya uhakika.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile jambo lingine, Kata ya Katanga, Kasuga pamoja na Kata ya Gorama ambapo Mheshimwa Mbunge ndipo anapotoka; Gwarama ni kweli kabisa hakuna kabisa mawasiliano, lakini hii Kata imeingizwa katika mradi wa Special Zone and Boarders ambapo utaanza kutekelezwa muda siyo mrefu.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo jingine Kata ya Katanga, Kasuga pamoja na Kata ya Gwarama ambapo Mheshimwa Mbunge ndiyo anapotoka. Gwarama ni kweli kabisa hakuna kabisa mawasiliano lakini hii Kata imeingizwa katika mradi wa Special Zone and Boarders ambapo utaanza muda si mrefu katika kutekelezwa. Mkandarasi katika eneo hilo amepatikana (Vodacom) na kwa hiyo tunaamini ndani ya miezi miwili, mitatu, ujenzi wa minara katika maeneo haya utakuwa umeshaanza na kwa hakika vijiji ambavyo viko katika Kata ya Katanga ambavyo ni vijiji viwili, Kata ya Kasuga vijiji vinne na Gwarama vijiji vitatu, tunaamini kwamba, wananchi wa maeneo haya watanufaika na huduma ya mawasiliano. (Makofi)

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini minara ya mawasiliano itapelekwa Kata za Nyamtukuza, Nyabibuye, Gwarama, Kasuga, Rugenge, Gwanumpu, Katanga na Magunzu?

Supplementary Question 2

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Bukura kwa maana ya Kirongwe, Roche, Goribe na Ikoma ni Kata zilizoko mpakani na Mheshimiwa Waziri nafikiri unazifahamu hizi, lakini ni Kata ambazo hazina huduma yoyote ya mawasiliano. Pamoja na kwamba, Mkandarasi amepatikana ninataka nijue commitment yenu ni lini Mkandarasi huyu ataanza ujenzi wa minara kwenye maeneo haya ya mpakani kati ya Tanzania na Kenya?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Chege, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari Mheshimiwa Mbunge jana tuliwasiliana na nikamhakikishia ndani ya miezi miwili mitatu tayari ujenzi utaanza. Ahsante sana.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini minara ya mawasiliano itapelekwa Kata za Nyamtukuza, Nyabibuye, Gwarama, Kasuga, Rugenge, Gwanumpu, Katanga na Magunzu?

Supplementary Question 3

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna changamoto kubwa sana kwenye mitandao ya simu, hasa Vodacom, ukiwa unaongea ina-stuck au inakoroma huku inaendelea ku-charge. Ningependa kujua nini tatizo katika mitandao hiyo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayoifanya kwa Mkoa wa Kagera, vilevile suala hili Mheshimiwa Waziri tayari ameshaunda timu ya kuzunguka nchi nzima kujiridhisha na huduma za mawasiliano nchini. Ni kweli kabisa kumekuwa na changamoto kama hizo, lakini tunaamini timu hii itakapokamilisha kazi yake basi tutachukua hatua stahiki ili wanchi wapate mawasiliano ya uhakika. Ahsante.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini minara ya mawasiliano itapelekwa Kata za Nyamtukuza, Nyabibuye, Gwarama, Kasuga, Rugenge, Gwanumpu, Katanga na Magunzu?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja la nyongeza: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, Mheshimiwa Naibu Waziri alifika Jimbo la Babati Vijijini kwenye Kata za Gidas na Ufana na kuahidi kwamba, ataleta minara ya mawasiliano. Je, ni lini ahadi hii itatimizwa ili wananchi wapate mawasiliano? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Baran Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa nimeshafika katika Jimbo la Babati Vijijini na katika Kata ambazo Mheshimiwa Sillo ameziongelea, tayari zimeingizwa kwenye mradi wa Tanzania kidijitali, tenda hiyo ilifunguliwa Tarehe 31 Januari, hivyo tunasubiri majibu ili tujue kwamba, ni Mkandarasi gani anapatikana kwa ajili ya vijiji hivyo. Ahsante.