Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 64 2023-02-03

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: -

Je, lini minara ya mawasiliano itapelekwa Kata za Nyamtukuza, Nyabibuye, Gwarama, Kasuga, Rugenge, Gwanumpu, Katanga na Magunzu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI, alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Buyungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kushirikiana na Kampuni ya Vodacom imetekeleza miradi ya kufikisha huduma za mawasiliano ya simu katika Kata za Nyamtukuza, Nyabibuye, Gwarama, Gwanumpu, Rugenge na Mugunzu. Miradi hii imetekelezwa kati ya mwaka 2016 na 2019 ambapo ujenzi wa minara katika Kata hizi umekamilika na inatoa huduma kwa teknolojia ya 2G na 3G.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Kata ya Katanga na Kasuga, Serikali itafanya tathmini ya hali halisi ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano Kata hizi katika mwaka wa fedha 2023/2024, ahsante.