Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, ni lini visima viwili vilivyochimbwa katika Mji wa Mpwapwa Mwaka 2021 vitaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza: Sambamba na visima hivi viwili kuchimbwa Mpwapwa Mjini, lakini mwaka wa 2021 kilichimbwa kisima kimoja katika Shule ya Sekondari ya Berege na mpaka sasa hivi akijaanza kufanya kazi: Je, ni lini kisima hiki nacho kitaanza kutoa huduma kwa wanafunzi wale wa Shule ya Sekondari ya Berege?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ni kwamba, kuna Miradi mitatu ya maji inatekelezwa katika Jimbo la Mpwapwa katika Kata ya Ving’hawe, Lupeta na Kijiji cha Igojiwani Kata ya Mima, lakini kasi ya utekelezaji wake imekuwa hafifu; je, nini tamko la Wizara kuhusu utekelezaji hafifu wa miradi hii? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge George Malima, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kusema, miradi yote ambayo imeanza kutekelezwa Waheshimiwa Wabunge ni lazima ikamilike.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu ambao utekelezaji wake Mheshimiwa Mbunge George ameuona ni hafifu, tutausimamia. Mradi namna mkataba umesainiwa tutajitahidi ukamilishwe ndani ya wakati. Kwa kisima kilichochimbwa shuleni, pia ni moja ya mikakati ya Wizara kuhakikisha maeneo kama haya ya shule au hospitali na vituo vya afya yanapata huduma ya maji safi na salama bombani. Hivyo kisima hiki kilichochimbwa pia tunakuja kukifanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, natoa agizo kupitia Bunge lako Tukufu, Watendaji wa Mkoa wa Dodoma wanaofanya kazi maeneo haya, wahakikishe wanatoa hizi sintofahamu haraka iwezekanavyo.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, ni lini visima viwili vilivyochimbwa katika Mji wa Mpwapwa Mwaka 2021 vitaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 2

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Wananchi wa Kijji cha Kigorogoro Kata ya Kibale kwa muda mrefu walikuwa na changamoto ya maji ya kisima. Kilichimbwa kisima, lakini kilipoanza kutoa maji, yakawa ni maji yenye chumvi kali wananchi wakashindwa kuyatumia. Naomba kuuliza swali: Ni lini wananchi wa Kijiji cha Kigorogoro watachimbiwa kisima kingine ambacho hakina maji ya chumvi, ukizingatia wapo kwenye ukanda wa Mto Kagera? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo ambalo kisima kimechimbwa na maji yakaonekana siyo rafiki kwa matumizi ya binadamu huwa tunayaacha na kutafuta mbadala wake. Ninaamini maeneo hayo watendaji wahusika wanaendelea kutafuta eneo mbadala na maji safi na salama lazima yaweze kuwafikia wananchi wa Kigorogoro.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, ni lini visima viwili vilivyochimbwa katika Mji wa Mpwapwa Mwaka 2021 vitaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 3

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kupeleka maji katika Kata ya Kwai, Kwekanga pamoja na Makanya?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Shekilindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kata hizi alizozitaja Mheshimiwa Mbunge Shekilindi, nimeongea naye juzijuzi na nimemhakikishia kwamba kazi hii tutaenda kuifanya. Tumeshakubaliana kwamba tunakwenda kuangalia mradi na tutahakikisha unatimizwa kufanyiwa kazi yake kwa wakati.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, ni lini visima viwili vilivyochimbwa katika Mji wa Mpwapwa Mwaka 2021 vitaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 4

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Napenda kuuliza, katika Wilaya ya Meatu tuna shida sana ya maji. Kwa Mkoa mzima wa Simiyu Wilaya ya Meatu inaongoza: Je, ni lini Serikali italeta maji safi na salama katika Wilaya Meatu ili wananchi wa kule wanufaike? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Minza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Simiyu una bahati sana. Una mradi mkubwa ambao unaenda kutekelezwa kwa kutumia kigezo cha mabadiliko ya tabia ya nchi. Mradi ule utafikisha maji maeneo ya Meatu, Maswa na maeneo yote yaliyo karibu kuhakikisha wananchi wanapelekewa maji safi na salama. Nafahamu Mheshimiwa Minza nawe pia umefuatilia sana suala hili, na nilifika Meatu na tunaendelea na kazi. (Makofi)

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, ni lini visima viwili vilivyochimbwa katika Mji wa Mpwapwa Mwaka 2021 vitaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 5

MHE. NOAH L. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kuna mradi wa vijiji tisa vya Oldonyo Sambu, Lengijave na Oldonyo-Wass ambao wanasumbuliwa na maji ya fluoride na imekuwa ikisuasua utekelezaji wake: Je, ni lini sasa Serikali itatoa fedha za kutosha kwa ajili ya kukamilisha mradi huu ambao wananchi wanateseka na maji ya fluoride? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Noah, Mbunge wa Arumeru, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tulipata tatizo na changamoto hii bado ipo, lakini sisi kama Wizara tayari tuna hatua mbalimbali tumeshazichukua na fedha tunatarajia mgao ujao. Mheshimiwa Mbunge nawe katika mradi ule tutapata. Lengo ni kuona tunatekeleza miradi mikubwa ambayo maeneo yake, maji yake chini hayana fluoride ili tuweze kunusuru watoto wanaoweza kuzaliwa na ulemavu na watu wote ambao wanateseka na maji yenye fluoride. (Makofi)

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, ni lini visima viwili vilivyochimbwa katika Mji wa Mpwapwa Mwaka 2021 vitaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 6

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona, niulize swali dogo moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndani ya Jimbo la Kibamba maeneo ya King’azi A, B na maeneo ya Manzese Malamba Mawili ni maeneo ambayo wananchi wanaendelea kukosa maji safi na salama kwa kutumia maji ya chumvi ya visima vifupi; na ahadi ya Serikali ni kujenga tenki kubwa la ujazo siyo chini ya lita milioni kumi pale Kilimahewa: Je, ni lini sasa Serikali itaanza kutekeleza mradi huo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mtemvu, Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tenki lipo kwenye hatua za mwisho kabisa kuja kuanza kutekelezwa, usanifu umekamilika. (Makofi)

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, ni lini visima viwili vilivyochimbwa katika Mji wa Mpwapwa Mwaka 2021 vitaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 7

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa nafasi ya swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna changamoto kubwa sana ya maji kwenye Kata ya Mtambula katika Jimbo la Mufindi Kusini; je, Serikali haioni wakati umefika sasa kuwapelekea maji sasa wananchi wa kata hii?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kihenzile, Mbunge wa Mufindi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tayari tumeona umuhimu na tupo katika taratibu za kuhakikisha hayo maeneo uliyoyataja Mheshimiwa Mbunge, tunayaletea maji safi na salama yakiwa bombani.