Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 61 2023-02-03

Name

George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: -

Je, ni lini visima viwili vilivyochimbwa katika Mji wa Mpwapwa Mwaka 2021 vitaanza kufanya kazi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Natany Malima, Mbunge wa Jimbo la Mpwapwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka fedha 2022/2023, Serikali imepanga kutekeleza ujenzi wa miundombinu ya usambazaji maji kutoka kwenye visima viwili vilivyochimbwa katika Mji wa Mpwapwa mwaka 2021. Kazi zilizopangwa kufanyika ni pamoja na ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilometa 48.8, ujenzi wa tenki lenye ujazo wa lita 200,000 na ujenzi wa vituo 18 vya kuchotea maji. Taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa Ujenzi zinaendelea na ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza mwezi Aprili, 2023 na kukamilika mwezi Aprili mwaka 2024. Kukamilika kwa mradi huu kutanufaisha wananchi wapatao 21,360 waishio kwenye Kata za Vihangwe na Mpwapwa Mjini.