Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

ASYA SHARIF OMAR K.n.y. MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kulinda miundombinu ya maji nchini?

Supplementary Question 1

MHE. ASYA SHARIF OMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake, lakini pia nina swali la nyongeza kwamba, wana mkakati gani wa kuwachukulia hatua wale wananchi ambao wanaharibu kwa makusudi miundombinu ya maji tukizingatia mahitaji ni makubwa ya wananchi mjini na vijijini? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tauhida ambalo limeulizwa kwa niaba yake: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nipokee pongezi lakini mkakati ambao tunaendelea nao ni kuchukua sheria. Sheria ziko bayana, kwa hiyo yoyote ambaye atakutwa sheria itafuata mkondo wake.

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

ASYA SHARIF OMAR K.n.y. MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kulinda miundombinu ya maji nchini?

Supplementary Question 2

MHE. JACQUELINE K. ANDREA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha usanifu wa matenki na michoro ya miundombinu katika Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria inayoenda katika Miji ya Urambo, Sikonge na Kaliua inaisha? Kwani usanifu huu ulitakiwa uishe Desemba, 2022 na ukizingatia Miji hii tayari ipo kwenye exemption ya kodi ili Mkandarasi aweze kwenda site na wananchi wa maeneo haya waweze kupata maji kwa urahisi. Ahsante sana.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jacqueline, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, usanifu ulipaswa kukamilika Desemba na sasa ni Januari, tuko mwishoni kabisa kukamilisha na lengo letu ni kuhakikisha dhumuni la kupeleka maji maeneo haya aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge tunakwenda kukamilisha kwa wakati.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

ASYA SHARIF OMAR K.n.y. MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kulinda miundombinu ya maji nchini?

Supplementary Question 3

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ikiwa wananchi wanapoharibu miundombinu ya maji wanachukuliwa hatua, je, ni ipi kauli ya Serikali pale ambapo miradi au miundombinu inapokuwa imekamilika watu wa mwenge wanapokuja kuzindua mradi, maji yanatoka lakini baada ya wiki mbili, hakuna maji tena, mnachukua hatua gani kwa udanganyifu wa wakandarasi wao ambao wanaidanganya jamii na hakuna maji na limekuwa ni jambo ambalo limezoeleka kwenye miradi mingi ya maji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Condester, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, udanganyifu wa aina hii Mheshimiwa Waziri alishaukomesha kwa kutuma vikosi kazi kuhakikisha mradi kama umezinduliwa unabaki kuwa endelevu. Nitafuatilia mradi huo anaouongelea Mheshimiwa Mbunge kujua tatizo ni nini ili kuhakikisha huduma iliyokusudiwa inapatikana.