Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 60 2023-02-03

Name

Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

ASYA SHARIF OMAR K.n.y. MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kulinda miundombinu ya maji nchini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tauhida Gallos Nyimbo Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu la Serikali ni kuhakikisha miundombinu ya maji inayojengwa inatunzwa na kulindwa ili kutoa huduma endelevu. Katika kutekeleza jukumu hilo kwa ufanisi, Serikali ilitunga Sheria Na.5 ya Mwaka 2019 ambayo inakataza kuharibu, kuvamia au kufanya shughuli za kibinadamu katika maeneo yenye miundombinu ya maji. Kupitia sheria hiyo ni kosa la jinai kuharibu miundombinu ya maji. Aidha, Serikali inaendelea kujenga uzio kwenye miundombinu ya maji ikiwemo matanki ya kuhifadhia maji na mitambo ya kutibu maji. Vilevile, elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa kulinda miundombinu ya maji nchini inaendelea kutolewa.