Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO K.n.y. MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia upatikanaji wa chakula cha bei nafuu kwa wananchi walioathirika na ukame nchini?

Supplementary Question 1

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa niulize swali moja la nyongeza. Korogwe Vijijini inazo Tarafa tatu ambazo zina jiografia ngumu sana, Tarafa ya Magoma, Mombo na Bungu. Mheshimiwa Mbunge Mnzava anataka kujua kwa nini Serikali isiweke kituo kingine cha pili katika eneo la Makuyuni ambako ndio Makao Makuu ya Halmashauri ili iweze kuhudumia Tarafa zilizobaki za Mombo na Mashewa.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu Mheshimiwa Reuben Kwagilwa, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo hilo la Makuyuni tutaipeleka hii selling point yetu na niwaondoe hofu wananchi wa Korogwe Vijijini watanunua mahindi kupitia eneo hilo la Makuyuni.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO K.n.y. MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia upatikanaji wa chakula cha bei nafuu kwa wananchi walioathirika na ukame nchini?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Tunaishukuru Serikali kwa kutoa chakula cha gharama nafuu. Je, Serikali ina mkakati gani kwa kaya ambazo hazina uwezo wa kununua chakula kwa sasa ili itoe chakula cha msaada?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, zipo taratibu ambazo huwa zinapelekea Serikali kufikia hatua hiyo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameiomba, nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge kupitia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, zipo taratibu za kwenda ofisi ya Waziri Mkuu ambayo pia wao wamekuwa wakiwasiliana nasi juu ya namna ya kupeleka chakula hiki cha msaada katika baadhi ya maeneo.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO K.n.y. MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia upatikanaji wa chakula cha bei nafuu kwa wananchi walioathirika na ukame nchini?

Supplementary Question 3

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Jimbo langu la Kalenga hasa Tarafa ya Kalenga tulipata shida ya mvua na tayari kata zile tumeshaleta maombi. Je, ni lini sasa Wizara itatupelekea chakula kwa haraka ili wananchi wangu wasife?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama maombi yake yamekwishawasilishwa ndani ya Ofisi ya NFRA, nataka nimhakikishie ndani ya siku mbili zijazo, mahindi yatamfikia katika jimbo lake.

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO K.n.y. MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia upatikanaji wa chakula cha bei nafuu kwa wananchi walioathirika na ukame nchini?

Supplementary Question 4

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa upandaji wa chakula unategemea gharama kubwa wanazozitumia wananchi katika kulima kwa maana ya kuchelewa kupeleka mbolea. Je, ni nini mkakati wa muda mrefu wa Serikali katika kuhakikisha wanapeleka mbolea kwa wakati ili wananchi waweze kulima kwa faida?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tumepata changamoto katika msimu huu wa upatikanaji wa mapema wa mbolea hasa ile ya kupandia, kukuzia na kunenepeshea. Nataka nimwondoe hofu kwa mfumo ambao tumeuweka kwenye msimu ujao, tutahakikisha wakulima wanapata pembejeo hizo kwa wakati ili waendane na msimu.

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO K.n.y. MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia upatikanaji wa chakula cha bei nafuu kwa wananchi walioathirika na ukame nchini?

Supplementary Question 5

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya yangu ya Nanyumbu inakabiliwa na njaa kubwa kutokana na shambulio la panya ndani ya Wilaya yangu. Tuliandika barua tupatiwe chakula cha bei nafuu hadi sasa hivi hatuna majibu. Je, ni nini kauli ya Serikali?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yahya Mhata, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nikimaliza kujibu maswali haya mimi na Mbunge tutakaa nione barua yake imefikia wapi, lakini nataka nimuahidi kwamba nitampelekea mahindi.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri aliyoyatoa Naibu Waziri, Mheshimiwa Antony Mavunde, nataka tuweke jambo hili vizuri kuhusiana na suala hili la njaa. Maeneo mengi Waheshimiwa Wabunge wamekuwa wakitoa taarifa kwamba, kuna shida ya upungufu wa chakula na kwa sababu hiyo sisi kwa mujibu ya Sheria ya Maafa, masuala ya chakula au upungufu wa chakula tunayachukulia kama ni maafa. Kwa tafsiri hiyo utaratibu wake ni kwamba, Halmashauri, Mkurugenzi anaandika barua kwa utaratibu wa kuleta kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu kupitia Mkoani, halafu barua ile inapelekwa kwa Waziri Mkuu, kwa ajili ya kupata kibali sasa ili chakula kile kiweze kutolewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu unaotumika sasa ni kama kila mmoja anaenda tu kiholela hivi, lakini kimsingi jukumu la kutoa kibali cha kwa ajili ya chakula ya bei nafuu au cha msaada ni jukumu la Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Waziri Mkuu itakachofanya ni kuwaelekeza Wizara ya Kilimo ili Wizara ya Kilimo sasa waielekeze NFRA kwenda kuangalia maeneo ya kupeleka, kuuzia kile chakula au mtu atakayenunua kile chakula na kwenda kukiuza kwa bei nafuu iliyopangwa. Kwa hiyo niwaombe sana ni kutokana na kukiukwa utaratibu huo, ndio maana mambo hayaendi pamoja na kuwa kwamba barua zimeandikwa.