Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE K.n.y. MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuiwezesha GST kufanya utafiti wa madini yanayohitajika kwenye soko la dunia kutengeneza nishati safi?

Supplementary Question 1

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, lakini ni kweli kwamba GST ina uwezo mdogo sana wa kiteknolojia kulingana na maendeleo makubwa teknolojia duniani. Sasa Serikali ina mkakati gani wa dharura kuiokoa GST kiteknolojia kwa sababu uwezo wake ni mdogo sana kiasi kwamba hata minerals zile certified mineral chemicals ambazo zinasaidia kuthibitisha ubora wa sampuli haina uwezo huo.

Je, Serikali ina mkakati gani wa dharura kuokoa GST?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia swali la pili, mpaka sasa Serikali imetoa leseni ngapi ambazo ziko kazini sasa hivi za madini ya kimkakati ambayo tunategemea GST itusaidie kuyabaini?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, la uwezo mdogo wa GST wa kufanya utafiti, naomba nimuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba GST kama taasisi ya utafiti itashirikiana na sekta binafsi. Kama nilivyoeleza kwenye jibu langu la msingi, tunazo kampuni mbalimbli ambazo ziko ndani na nje ya nchi ambazo zinafanya kazi ya utafiti kusaidia Taifa letu. Hivi sasa tumeshazungumza na kampuni mbalimbali kubwa duniani kwa akjili ya kufanya utafiti huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kwamba tumetoa leseni ngapi; tumeshatoa leseni kadhaa, naweza nisijue kwa idadi, lakini madini yote ya mkakati anayoyafahami iwe nickel, iwe graphite iwe rare earth, iwe helium na kadhalika; yote haya kuna leseni na makampuni mbalimbali yanaendelea na utafiti hapa nchini. Kwa hiyo naomba nimuhakikishie, demand ya madini mkakati ambayo anahitaji sasa hivi ni jambo ambalo halikuwa la muda mrefu, na wawekezaji wengi walikuwa busy na madini mengine. Sasa hivi muelekeo mkubwa ni kufanya haya madini mkakati na kampuni nyingi zipo zinafanya hizi kazi. Baada ya muda ataona migodi mingi inajengwa kama ambavyo kabanga inajengwa.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE K.n.y. MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuiwezesha GST kufanya utafiti wa madini yanayohitajika kwenye soko la dunia kutengeneza nishati safi?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Katika Jimbo la Sikonge wananchi wangu wanaendelea kuamini kwamba katika Mlima wa Kipanga, Milima ya Kisanga na Mapori ya Ipembampazi kuna madini; na hili suala limeulizwa tangu enzi za Mheshimiwa Said Nkumba akiwa madarakani.

Je, Serikali itakuja lini sasa kuja kufanya utafiti ili kuitikia wito wa wananchi kwamba kule kuna madini?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kakunda, Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba yapo maeneo mbalimbali Mkoa wa Tabora ambayo yanaaminika kuwa na madini na bahati mbaya hayajafanyiwa utafiti wa kina. Taasisi yetu ya utafiti GST iko katika Mikoa ya Kusini. Nataka nimhakikishie, baada ya kumaliza mzunguko wa Kanda ya Kusini tutawapeleka na Mkoa wa Tabora, ikiwemo eneo la Sikonge ili waweze kufanya utafiti wa awali.