Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Madini 56 2023-02-03

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE K.n.y. MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuiwezesha GST kufanya utafiti wa madini yanayohitajika kwenye soko la dunia kutengeneza nishati safi?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jesca David Kishoa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa ni asilimia 16 tu ya nchi yetu ndiyo imefanyiwa utafiti wa kina kubaini aina na kiasi cha madini mbalimbali yanayopatikana kwa kutumia teknolojia ya urushwaji wa ndege (High Resolution Airborne Geophysical Survey). Teknolojia hiyo hutoa picha ya chini ya ardhi inayoonesha mikondo na miamba inayobeba madini ya aina mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Wizara ya Madini imekwisha andaa mpango mkakati wa utafiti utakaowezesha kutafiti asilimia 50 ya nchi yetu ili kupata na taarifa za kina ikiwemo za madini ya nishati safi. Mpango huo umekwisha kuainishwa na maeneo ya kipaumbele kulingana na aina ya madini yanayohitajika zaidi nchini kwa sasa. Ili kufanikisha azma hiyo, Wizara inajadiliana na sekta binafsi zinazoonesha nia ya kushirikiana na GST ili kuwezesha utafiti wa kina wa madini mkakati wa teknolojia ya utafutaji, uvunaji na uongezaji thamani madini ya mkakati kwa kuwa ni gharama kubwa sana.