Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa mradi wa Liganga na Mchuchuma?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa usemi wa majadiliano unaendelea na umekuwa wimbo wa muda mrefu; na kwa kuwa mradi huu nji muhimu sana kwa Taifa letu ikiwa ni sambamba na kupata ajira 5,000 zilizo rasmi na zisizo rasmi 25,000 na vile vile tunatambua kwamba, baada ya miaka 15 makaa ya mawe yatakuwa hayana soko tena duniani kutokana na teknolojia zinazoendelea.

Je, Serikali inaweza ikatupa muda specific time lini mtamaliza majadiliano na muwekezaji huyu ili tuende awamu nyingne na mradi huu, uweze kutekelezeka kwa maslahi ya wananchi wa Tanzania?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Neema William Mgaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mtakumbuka wakati tunawasilisha Taarifa ya Kamati kwenye Bunge lako tumeeleza kwa kirefu jinsi ambavyo Serikali imechukua jitihada za maksudi kuhakikisha tunakamilisha mapema majadiliano haya, lakini changamoto ilikuwa kwa upande wa wawekezaji hawa ambao tuliingia nao mkataba kabla. Hata hivyo tunaamini katika mwaka wa fedha ujao (2023/2024), In Shaa Allah, tutaweza kukamilisha kwa sababu tayari tuko kwenye hatua nzuri zaidi ili tuweze kufikia hatma ya majadiliano haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.