Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 55 2023-02-03

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa mradi wa Liganga na Mchuchuma?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imedhamiria kuona mradi unganishi wa Linganga na Mchuchuma unatekelezwa mapema iwezekanavyo. Serikali imefanya uthaminishaji mpya katika eneo la mradi baada ya ule wa kwanza kwisha muda wake kwa mujibu wa sheria na zoezi la kuhuisha tathmini ya taarifa za wananchi lilikamilika mwezi Disemba, 2022. Pia tumehuisha majadiliano na mwekezaji wa mradi ili kuhakikisha majadiliano yanakamilika kwa wakati pasipo kuleta hasara kwa Taifa na kutoa fedha za kutengeneza miundombinu kwa maana sehemu korofi za barabara katika eneo la Milima ya Kemilembe Mchuchuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua umuhimu mkubwa wa Mradi huo kwa Taifa letu, napenda kuwahakikishia kuwa juhudi zinazofanyika hivi sasa zitawezesha utekelezaji wa mradi huo haraka.

Mheshimiwa naibu Spika, nakushukuru.