Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, wananchi wa Vunjo wamenufaika vipi na Mifuko ya Uwezeshaji ya Wajasiriamali kama NEEC, NEDF, SELFU na TAFF?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, inasikitisha sana, nashukuru sana ametoa majibu ya swali hilo. Hata hivyo inasikitisha sana kwamba mifuko hii inajikita kwenye majiji na kwenye manspaa ambazo zina uwezo mkubwa kwa zile asilimia zao 10 kutoa mikopo kwa vijana, wanawake na walemavu. Wamejikita huko sasa, ni ile ile dhana kwamba watu wanaohitaji zaidi ni vijijini lakini hii mifuko hailengi wale wa vijijini.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuhakikisha kwamba mifuko hii inabadilisha misimamo yake au mitizamo yake na kulenga zaidi Halmashauri kwenye wilaya za vijijini? Hilo ni la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, je, Serikali haioni umuhimu wa kuunganisha mifuko hii ili kupunguza gharama za uendeshaji na pia kutoa usawa zaidi na ufanisi katika kutoa mikopo yake?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Kimei, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika moja ya mikakati ambayo tunaifanya Serikali ni kuona namna gani mifuko hii ya uwezeshaji itawasaidia zaidi wananchi walioko katika maeneo ya vijijini na ndio maana moja ya mifuko hii au pesa zinazotolewa kwa wajasiliamali ile asilimia 10 ina gusa katika Halmashauri zote ambazo zinagusa pia vijijini. Pia zaidi tutaangalia na hii mifuko mingine ikiwemo ya NEDF, SELFU na TAFF iweze kufika kule vijijini kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameshauri.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la pili tayari tumeshaanza na kazi hiyo inafanyika, kuona namna ya kuunganisha mifuko inayotoa fedha au inahudumia shughuli zinazofanana na taarifa hiyo tayari inakamilika iko kwenye hatua za mwisho kuona mifuko ipi itaunganishwa ili kupunguza wingi wa mifuko hii, ambayo inahudumia watu wanaofanana.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, wananchi wa Vunjo wamenufaika vipi na Mifuko ya Uwezeshaji ya Wajasiriamali kama NEEC, NEDF, SELFU na TAFF?

Supplementary Question 2

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali inaonesha kusua sua kwa ufanisi wa mifuko hii, na ni tangu Bunge la Kumi na Moja tumekuwa tukizunngumza kuhusu kuunganisha mifuko ya uwezeshaji wananchi kiuchumi, mifuko ya ujasiriamali.

Je, ipi kauli ya Serikali, kwa kutumia muda mrefu kiasi hiki, wanasemaje kuhusiana na kuharakisha mchakato kwa sababu ni fedha za Serikali zinazoenda huko?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Nusrat Hanje, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema Serikali tumeshaanza na tumeshafika hatua ya mwisho. Naamini katika mwaka wa fedha ujao kutakuwa na taarifa kamili ya nini mfuko huu pia utapunguzwa. Kwa sababu tuna mifuko zaidi ya 72 lakini kati ya hiyo tisa ni ya sekta binafsi, 63 ndiyo ya Serikali. Kwa hiyo, tunaanza kwanza hii ya Serikali 63 tuone namna gani tunapunguza ili iweze kuwa na tija kama ambavyo Bunge lako limeendelea kushauri, nakushukuru.