Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 54 2023-02-03

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: -

Je, wananchi wa Vunjo wamenufaika vipi na Mifuko ya Uwezeshaji ya Wajasiriamali kama NEEC, NEDF, SELFU na TAFF?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Jimbo la Vunjo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mifuko na programu za uwezeshaji zimetoa manufaa makubwa katika kuwezesha mikopo, ajira, kipato kwa wananchi wakiwemo wananchi wa Vunjo. Mifuko na programu za uwezeshaji zimetoa jumla ya mikopo yenye thamani ya shilingi trilioni 5.68 tangu kuanzishwa kwake. Mathalani katika Jimbo la Vunjo, kwa kipindi cha mwaka 2019/2020 hadi 2021/2022 mfuko wa NEDF umetoa mikopo 11 yenye thamani ya milioni 25.2 na Mfuko wa TAFF umetoa ruzuku yenye thamani ya shilingi milioni 20, nakushukuru.