Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya kilimo kuwa kipaumbele cha kwanza cha Taifa kwa kupunguza bei ya mbolea?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali iliahidi Bilioni 150 katika kutoa fedha kwenye ruzuku na imetoa Bilioni 50 tu, sasa haioni sababu ya kuongeza hiyo Bilioni 100 iliyobaki ili mbolea iweze kupatikana kwa wingi zaidi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, tunaomba Serikali iongeze speed kusajili mawakala ambao watasaidia mbolea ipatikane kwa wingi, kwa maana mawakala waliopo ni wachache na inakuwa na uzito mkubwa sana wa kupeleka mbolea mpaka kule vijijini. Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza kuhusiana na fedha za ruzuku, kama ambavyo yalitolewa majibu na Mheshimiwa Waziri hapa, fedha zinaendelea kuletwa kwa ajili ya kushughulikia suala la ruzuku ya mbolea na nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba yale yote ambayo tuliyaahidi tutayasimamia ili wakulima wetu waweze kupata mbolea na Wizara ya Fedha wameendelea kushirikiana nasi kwa ukaribu sana.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu speed ya usajili wa mawakala, tumetoa maelekezo hivi sasa ya kuwataka Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa katika maeneo amabako mbolea hazifiki kwa wakati na wakulima wako mbali, kuanza kusajili vituo vingine vipya ili kuwarahisishia huduma wakulima na mbolea hizo ziweze kuwafikia kwa uharaka. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba zoezi hilo linaendelea na usajili umeendelea kusajili vituo vingine vipya.

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya kilimo kuwa kipaumbele cha kwanza cha Taifa kwa kupunguza bei ya mbolea?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ninaishukuru Serikali kwa mbolea ya ruzuku lakini kwa kuwa mbolea hii tangu tumepitisha bajeti hapa, maeneo kama ya Kagera ambao tunakuwa na msimu wa kilimo umeshapita na mbolea haikupatikana kwa wakati kwa sababu mawakala hawapo kabisa.

Je, ni nini kauli ya Serikali kwa wananchi hususan wa Wilaya ya Bihalamuro ambao wamekosa kabisa mbolea hii ya ruzuku ili kipindi cha msimu unaofuata waweze kuwa na matumaini ya kupata mbolea hii kwa wakati?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ezra Chiwelesa, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tulipata changamoto ya mfumo wa usambazaji, ambao hivi sasa tumeendela kuurekebisha na hivi sasa tumeruhusu pia usajili wa vyama vya ushirika, kuwa kama sehemu ya wasambazaji wa mbolea vilevile na vyama vya wakulima vilivyosajiliwa na pia tutatumia baadhi ya maghala yaliyokuwa katika mradi wa MIVARF kama sehemu ya usambazaji wa mbolea hizi. Kwa hiyo, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba katika kipindi kinachokuja changamoto hii haitajirudia tena, tutahakikisha kwamba mbolea inawafikia wakulima kwa wakati lakini katika maeneo yao walipo pia.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya kilimo kuwa kipaumbele cha kwanza cha Taifa kwa kupunguza bei ya mbolea?

Supplementary Question 3

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Msheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kumekuwa na malalamiko na changamoto kadhaa kwa upatikanaji wa mbolea na bei kuwa juu. Je, Serikali ina mpango gani wa kushajihisha kilimo hai ambacho kinatumia mbolea asilia na kina gharama nafuu ambazo pia hakitumiii kemikali na vilevile ina uwezo wa kuhuisha afya ya udongo na afya zetu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asha Juma, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara tumekuwa tukifanya jitihada mbalimbali za kuwakaribisha wadau mbalimbali wanaozalisha mbolea ambao ni organic na habari njema tu ni kwamba nilipata nafasi ya kwenda katika maonesho ya kilimo hai Ujerumani na tukakutana na wawekezaji wengi ambao wameonesha nia ya kuja uwekeza hasa katika Mkoa wa Lindi na Mtwara. Hivyo, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba ni sehemu ya mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba mbolea hii pia inazalishwa ili kupunguza gharama hii kwa wakulima.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya kilimo kuwa kipaumbele cha kwanza cha Taifa kwa kupunguza bei ya mbolea?

Supplementary Question 4

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Zao la pamba ni kati ya mazao ya kimkakati hapa nchini lakini wakulima wake bado wanazalisha kilo 300 mpaka 400 kwa heka moja.

Je, ni nini mkakati wa Serikali sasa kwa wakulima hawa waweze kuzalisha kilo 500 mpaka 1,000 kwa heka moja?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika napenda kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Cherehani, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, anachokizungumzia Mbunge hapa ni tija na sisi tumejipanga katika Wizara kuhakikisha wakulima wetu wanalima kwa tija. Kwanza, kabisa kuwasaidia kupata viuatilifu sahihi; pili, kuwasaidia kupata teknolojia za kisasa za kilimo cha pamba; na tatu, ni kuhakikisha kwamba wanajifunza kanuni bora za kilimo kama ambavyo hivi sasa tumeona kule kupitia TARI na Balozi wa Pamba juu ya mfumo mpya wa spacing ambao umesaidia sana kuongeza uzalishaji katika zao la pamba.

Kwa hiyo, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba, tunatambua changamoto hizo na tumejipanga kuhakikisha kwamba mkulima wa pamba anazalisha kwa tija.